Share this:


UFAHAMU NA UFUPISHO

UFAHAMU
Ufahamu Ni hali ya kulijua na kulielewa jambo kwa usahihi na kuweza kulielezea kwa ufasaha bila kupoteza maana yake ya msingi
Au. Ni kujua na kuelewa jambo na kuweza kulifafanua
Madhumuni ya kufundisha ufahamu ni kumwezesha mwanafunzi kuelewa mambo mbalimbali kwa njia ya lugha pamoja na kukuza ustadi wake katika kuzungumza kusoma na kuandika
Aina za ufahamu
  • Ufahamu wa kusoma
Ni kuzingatia maana ya neno sentensi na habari yote. Msomaji lazima aweze kutambua mpangilio wa herufi maneno na tarakimu na kuzitofautisha
Upo usomi wa aina mbili
(I) Kusoma kimya
(II) Kusoma kwa sauti
Usomaji wa makini na kina katika habari husika
KUSOMA KIMYA NA KWA HARAKA
Ni njia ambayo msomaji anapitisha macho kwenye maandishi bila kutilia makini na sio kwa kina
Ili kufaulu kwa habari kwa usahihi, maswali yanayotokana na habari ya kusoma sharti azingatie mambo yafuatayo
  • Kuwa mtulivu na makini
Msomaji anapaswa kuwa mtulivu na makini katika kile anachokisoma kwa kufanya hivyo huweza kuelewa vizuri mada kuanzia utangulizi wake hadi hitimisho na bila kuruka baadhi ya aya
  • Kuelewa maana ya maneno na misemo
Zipo njia mbili za kupata maana ya maneno katika habari
  • Kwa kutumia kamusi
  • Kwa kuzingatia muktadha (mazingira) ambamo neno au maneno yametumika. Hapa tunapata kama lilivyotumika kwenye kifungu cha habari kwa kuwa neno moja huweza kuwa na maana nyingi. Msomaji anapaswa ajizoeshe kupata maana kama ilivotumika katika habari
  • Kubuni mawazo
Kwa kawaida aya moja huzungumzia wazo kuu moja. Msomaji anatakiwa abainishe wazo kuu kwa kila aya.
Msomaji hanabudi kuzingatia mbinu za kujiuliza katika kubainisha wazo katika aya hatimaye kiini cha habari nzima ambacho hutoa picha ya aya zote
  • Kubainisha matumizi mengine ya lugha
Katika nakala/ habari kuna kuwa na matumizi mbalimbali ya lugha kama vile nahau na misemo, methali, tamathali za semi, ishara/taswira
Kujibu maswali kutokana na taswira uliyosoma inabidi uzingatie mambo yafuatayo
  • Soma nakala inayohusika
  • Ukishasoma, soma maswali uliyoulizwa ili kujua kinachotakiwa
  • Ukishajua kinachotakiwa rudia kusoma nakala yote, safari hii kwa makini zaidi huku ukijitahidi kupata mawazo muhimu ya maswali yaliyoulizwa
  • Msomaji katika hatua hii anaweza kutumia kalamu ya risasi kuweka alama katika sehemu anayodhani ni jibu sahihi
  • Baada ya kusoma nakala hiyo na kuweka alama majibu yako sasa msomaji anaweza kujibu maswali
KUSOMA KWA SAUTI
Ni aina ya usomaji ambao humwezesha msomaji kupata ujumbe na kuweza kutamka lafudhi ya Kiswahili
  • Ufahamu wa kusikiliza
Ni ule ambao muhusika anaupata kwa kusikiliza habari fulani. Inawezekana kupata kwa kusimuliwa au kusomewa
Ili kupata ufahamu kutokana na habari unayosikiliza lazima msikilizaji azingatie mambo yafuatayo;-
  • Kusikiliza kwa makini ili kuelewa wazo kuu
  • Kuhusisha mambo muhimu na habari inayosimuliwa
  • Kujua matamshi ya mzungumzaji
  • Kubainisha mawazo makuu
Mambo ya kuzingatia katika ufahamu wa kusikiliza
  • Kubaini mawazo makuu
Msimulizi akizungumza huwa ana ujumbe anaotaka uwafikie watu. Wakati mwingine hupanga ujumbe huo kwa namna nyepesi ili msikilizaji aupate kwa haraka.
Mara nyingine huchanganya wazo zaidi ya moja kutoka aya moja lakini mawazo hayo yanakuwa yanahusiana.
Ili msikilizaji aweze kubaini wazo kuu, atalazimika kusikiliza kwa makini
  • Kubaini maana ya maneno na misemo
Katika habari ambayo mtu anapata katika kusikiliza aghalabu kuna maneno magumu. Hivyo maana ya maneno itapatikana kulingana na matumizi (maana iliyokusudiwa) kama msomaji ameshindwa kupata maana anashauriwa kutafuta katika kamusi ya Kiswahili
  • Kusikiliza kwa utulivu
Ni wajibu wa msikilizaji kusikiliza kwa utulivu maelezo ya msomaji. Mbinu hiyo itamwezesha kuelekeza fikra zake kwenye maelezo yanayotolewa na hivyo kuweza kuelewa mada vizuri pamoja na maswali kwasababu kuna wengine hawamudu vizuri matamshi sahihi ya Kiswahili
Mfano; raha – laha
Fedha – feza

  • Kujibu kwa ufupi
Baada ya kubaini majibu/ jibu la maswali/swali unatakiwa kujibu kwa kutumia maelezo machache tu. Maelezo hayo sharti yawe tu yanahusiana na kipengele kinacholengwa na swali.
UFUPISHO
Ni maelezo mafupi yaliyoandikwa kutokana na habari ndefu bila kupoteza maana ya msingi ya habari hiyo.
Ufupisho husaidia katika shughuli mbalimbali kama,
  • Husaidia wakati wa kudondoa hoja kutokana na mihadhara, hotuba n.k
  • Husaidia katika uhariri wa habari
  • Hutumika katika kuandika kumbukumbu za kila siku
  • Huokoa fedha kama vile upelekaji wa simu za maandishi
  • Hutumika wakati wa kutayarisha ripoti na kumbukumbu za mikutano
Hatua za kufupisha habari
  • Kuisoma au kuisikiliza habari kwa makini ili kuelewa vizuri.
  • Kutambua au kubaini mawazo makuu yanayojitokeza katika kila aya.
  • Kuyaunganisha mawazo makuu na kuiandika au kuielezea habari hiyo kwa maneno yako mwenyewe
  • Kuhesabu idadi ya maneno ya ufupisho ili kuyapunguza ikiwa yanazidi idadi inayotakiwa
  • Kuandika idadi ya maneno mwisho wa ufupisho upande wa kulia wa chini kidogo
Wakati wa kufupisha ni muhimu kuzingatia njeo, kauli na nafsi kama ilivyotumiwa katika matini ya awali. Kwa kawaida habari hufupishwa hadi kufikia theluthi moja 1/3 ya maneno ya matini awali
Ufupisho pia hufanywa kwa kubaini kichwa cha habari kwani ndicho kiini cha habari hupatikana baada ya kutambua mawazo makuu ya kila aya na kuyafupisha
Kichwa cha habari kinatakiwa kisizidi maneno matano.

VITABU TEULE VYA FASIHI

UCHAMBUZI WA RIWAYA.
Jina la kitabu: TAKADINI
Mwandishi: BEN J. HENSON
Wachapishaji: METHEWS BOOKSTORE AND STATIONERS
Mwaka: 2004
A: UTANGULIZI
Takadini ni riwaya inayoeleza maisha ya jamii za Kiafrika na tamaduni zao. Hii ni desturi ambayo imeandikwa kulenga watu au jamiii ya watu wanaokumbatia mila na desturi zilizopitwa na wakati. Riwaya hii imeelezea namna jamii nyingi za Waafrika walivyowakandamiza au kuwanyanyapaa watu waliozaliwa na ulemavu katika jamii.
Mwandishi ametumia ‘Zeruzeru’ Kama mfano tu wa wahanga wa mila na desturi zilizowataka wanajamii kuwafutilia mbali walemavu hao katika uso wa dunia hii.
Mwandishi amejaribu kuonesha baadhi ya mila zilizopo katika Jamii kuwa hazifai kuendelea kutumiwa kwani hazizingatii utu wa mtu. Tofauti za rangi au upungufu wa viungo vya mwili si kigezo cha kutotambua utu wa watu.
Katika riwaya hii, mwandishi anatuonesha maisha anayopitia Takadini kuwa yalijaa unyanyapaa, ubaguzi, uonevu na kudharauliwa n.k. Kuzaliwa kwa Takadini kulisababisha mgawanyiko mkubwa sana katika jamii kwani hakutakiwa na jamii nzima isipokuwa mama yake Sekai tu ambaye alilazimika kwenda uhamishoni ili kunusuru maisha ya mtoto wake. Takadini anatengwa na watoto wenzake, watu wazima na jamii nzima. Anakua katika maisha ya kutengwa sana.
Hata hivyo Sekai na baba Chivero ndio walibaki kuwa wazazi na marafiki wa kweli maishani mwake.
Je, Zeruzeru (sope) hakuwa na haki ya kuishi kama jamii yake ilivyoamini? Je, Zeruzeru hana nafasi katika ujenzi wa jamii mpya kama walivyo watu wengine?
Takadini katika maisha yake anatupatia majibu ya maswali yote haya. Takadini kama Zeruzeru (sope) aliweza kufanya shughuli mbalimbali kwa umaridadi kama watu wengine au hata kuwazidi watu wasiokuwa na ulemavu. Takadini alionyesha kuwa sope ni mtu kama walivyo watu wengine na kwamba wana hisia na haki ya kupenda na kupendwa. Takadini aliangukia katika penzi la dhati la Shingai.
Walifanikiwa kupata mtoto ambaye hakuwa Zeruzeru.
Kwa nini Zeruzeru wauliwe?
Kwa nini Zeruzeru watengwe?
Kwa nini Zeruzeru wadharauliwe?
Kwa nini Zeruzeru wavuliwe utu wao?
Hakuna sababu ya msingi inayoweza kuhalalisha unyama wanaotendewa walemavu wote. Ni baadhi ya mila na desturi ndizo zimejaribu kuhalalisha hayo kwa muda mrefu. Jamii sasa inabadili mtazamo wake kuhusu zeruzeru na walemavu wote wanalindwa na kupewa fursa sawa na wengine ili utu na heshima zao ziweze kutambuliwa na kuzingatiwa na jamii nzima.

PITIO LA KITABU
  1. Familia ya mzee Makwati
Mzee Makwati alikuwa na wake wanne na wote aliwapenda sana. Mke wa kwanza alikuwa Sekai wa pili aliitwa Pindai, watatu Dadirai na wa mwisho ambaye alikuwa ni mdogo kuliko wote aliitwa Rumbiozai.
Katika familia hii wake wa mzee Makwati wanaonekana wakibaguana wenyewe kwa wenyewe na pia wanakuwa hawaelewani huku wivu ukiwatawala.
Mfano, Mke wa kwanza alikuwa ni rafiki mkubwa wa mke wa pili na ndivyo hata mke wa tatu alikuwa rafiki wa mke wa nne ambaye ni wa mwisho. Sekai ni mke wa kwanza wa mzee Makwati na aliishi kwa miaka tisa pasipo ujauzito na hatimaye kupata ujauzito. Lakini ujauzito ule wa Sekai unaibua minong’ono ya chinichini kwa wake wenza na walimkejeli kwa kumwambia “ni ndama wangapi ambao ng’ombe wake mzee amepata kwa miaka minne iliyopita? Rumbiozai alihoji oh amezaa watatu kwa miaka minne. (Dadirai alijibu kwa sauti ya juu na Sekai akasikia).
Kuwepo kwa imani za kishirikina hasa pale walipohisi ni kwa vipi Sekai anaweza kuishi muda mrefu pasipo kuwa na mtoto na mumewe. Pia tunaona kuwa chakula cha jioni kinaandaliwa na wake wote wanne wa mzee Mkwati
lakini mzee Mkwati baada ya kuonja vyakula vyote ndipo anaishia kula chakula kilicholetwa na Sekai.
Hatimaye Sekai anapata ujauzito na yeye analiona kitendo kile ni cha ajabu kwa kubeba mtoto mchanga katika mwili wake na anajiuliza je mtoto huyu atakuwa wa kike au wa wakiume na atakuwa na kasoro na mbaya zaidi kiumbe hicho kitakuwa binadamu au la maana ameshawahi kusikia kuhusu wanawake waliojifungua juu ya ujauzito ule wa mkewe. Sekai. Anatabiri juu ya ujauzito ule kuwa ni wa mtoto wa kike lakini mzee Makwati anakuja juu na kumwambia mkewe kuwa yeye haitaji tena mtoto wa kike bali anahitaji mtoto wa kiume. Hivyo Sekai anamhakikishia mumewe kuwa mtoto huyo atakuwa wa kiume na tena shupavu kama mzee Makwati mwenyewe.
Pia tunaona juu ya msimamo alionao mzee Makwati allipokuwa akimwambia mkewe kwa kumuuliza, “Je, wewe siyo mke wa kwanza wa penzi la kweli? Vipi aibu yako isiwe yangu pia? Je, siyo Mimi niliyesimama imara kati ya wazazi wangu na wewe kwa miaka hii yote”? Na mkewe akajibu “Natambua hili sana maana umepigana nao kwa muda mrefu, nawe ulikataa kunirudisha kwetu maan hapo sina dada wa kuchangia naye mkeka, nashukuru sana mume wangu kwa kunifichia aibu yangu.
  1. Furaha kubwa kwa Sekai
Muda wa mwisho wa ujauzito wa Sekai ulikaribia na ndipo rafiki yake, mke mwenza Pindai anamsaidia kazi za nyumbani. Amai Pedzisai ni mzee aliyekuwa kipenzi cha Sekai na aliweza kuwa karibu sana na Sekai mpaka alipokaribia kujifungua. Sekai alipata maumivu makubwa ya uchungu kuliko maumivu yote aliyowahi kuyapata, mbali na maumivu hayo lakini alitarajia kuwa na furaha kubwa siku chache zijazo.
Hatimaye Sekai alijifungua mtoto wa kiume. Taarifa hii ilipelekea furaha kubwa kwa mume Makwati. Lakini mtoto huyu aliyezaliwa aligundulika kuwa ni Sope(zeruzeru) na hata Sekai aligundua hilo na ndipo Sekai anaonyesha kuwa na woga juu ya mtoto yule lakini kwa upande mwingine anaonyosha ujasiri wake kwa kusema, “Lazima mtoto aishi maana nimesubiri kwa muda mrefu na nimeshateseka sana juu yake, hivyo mtoto huyu ni wangu na wala sitamuachia mtu”. Ambuya alimwambia, “hujui ulisemalo hivyo usihofu maana uzazi umeshafunguka na watafuata watoto wengine”.
Mzee Makwati anapata taarifa juu ya mtoto aliyezaliwa kuwa ni sope(zeruzeru) naye anaonyesha kuchukizwa na kiumbe hicho na alihoji kwa mkewe katika hali ya maswali ya mfululizo mfano, “Huo ni uchawi au ni laana ya mizimu? Na kwa nini huyo Sope yungali nasi”?, maswali haya yalimtatiza Sekai katika kuyajibu, na ndipo mzee Makwati alitoa suluhisho kwa kusema wazee ndio watatoa suluhisho la kuwepo au kutokuwepo kwa mtoto yule.
Mganga mashuhuri aitwaye Zviyedzo anashirikishwa katika kutatua tatizo lile la mtoto ambaye ni Sope.
  1. Gumzo dhidi ya mtoto Zeruzeru
Kuzaliwa kwa mtoto wa ajabu pale kijijini kulizua gumzo kubwa na habari kuhusu mtoto huyo zilienea kwa haraka kijijini hapo hivyo kila mtu alishikwa na butwaa.

Wake wenza na Sekai walimkejeli kwa maneno mabaya na wengine walionyesha chuki zao lakini ilikuwa tofauti kwa Pindai ambaye alionyesha upendo kwa mke mwenza huyo.
Pindai na Pedzisai walimtembelea Sekai na waliweza kujadili mambo mbalimbali zikiwemo mila na desturi za hapo kijijini . Pia waliweza kumuuliza Sekai ni kwanini aliendelea kuwa na mtoto yule na hivyo walimueleza kuwa alikuwa akipinga mila na desturi zao hapo kijijini na kutojulikana kwa ufumbuzi wa mtoto yule kulimpelekea Sekai kuwa na mawazo mengi yasiyo na kikomo, hata mzee Makwati pia naye alikuwa na mawazo mengi juu ya mtoto yule aliyezaliwa akiwa Sope.
Mzee Makwati anakasirika kwa kuona mtoto yule aliye Sope na anamshutumu mkewe labda ametembea na mwanaume mwingine hivyo amevunja mila ma desturi zao. Sekai aliumizwa sana na tuhuma hizo
maana alijiona hana maana tena mbele ya mumewe na anajihisi aliyetelekezwa zaidi wakati huo. Mtihani mkubwa ulikuwa kwa Sekai na alichokuwa akisubiri ni hukumu kutoka kwa wazee juu ya yeye na mwanae kuendelea kuishi au kutoendelea kuishi.
Mikakati mikubwa ilipangwa na Sekai ili kunusuru kifo chake pamoja na mwanaye hivyo alipanga kutoweka upesi katika kijiji kile, lakini uamuzi wake ulihitaji ujasiri mkubwa na ungeweza kuleta matumaini ya kuishi maisha mapya kwa Sekai na mtoto wake.
Alfajiri ilipofika, Sekai alijiandaa kwa safari, alifungasha vitu vyote ambavyo vilikuwa muhimu katika safari yake na bila kusahau zana za kujilinda dhidi ya wanyama wakali ambazo ni ngao na mkuki. Kabla ya kuanza safari, Sekai aliketi na kuiambia mizimu matatizo yake na akaomba akingwe na mambo yote ya hatari mbele ya safari yake.
Wakati alipo wasiliana na mizimu, punde jina likamjia moyoni aliweza kumpa jina hilo mtoto wake ambalo ni TAKADINI, ni jina ambalo hakuwahi kulisikia mahali popote pale. TAKADINI maana yake ni “Sisi tumefanya nini?” Jina hili lilisawiri vyema mambo yote yaliyomtokea Sekai wakati wa uzazi wa mwanae na huu wa sasa wenye hatari zaidi kwake.
  1. Safari ya Sekai
Alfajiri na mapema Sekai alianza safari yake kimyakimya toka kibandani mwake.
Alimchukua mwanae Takadini na vifurushi alivyoviandaa kwa ajili ya safari bila kusahau mkuki na ngao.
Sekai alivuka milima, mabonde na tambarare akielekea asikokujua. Kijiji alichotoka Sekai aliacha gumzo kubwa juu yake ambapo wengine walisema, “Labda alikwenda kujinyonga au amekwenda kujitosa majini.
Habari za kutoweka kwa Sekai zilienea kijiji kizima na ndipo Mtemi Zvedi aliitisha mkutano ili kujadili ni wapi aloko kwenda Sekai na ndipo Mtemi alitoa agizo la kumtafuta Sekai popote pale kuzunguuka kijiji chote.
Katika safari yake Sekai anakutana na mzee Chivero na anamueleza mkasa wote uliompata na lengo la yeye kutoroka. Mzee Chivero anamkaribisha Sekai katika kijiji chake na anamtambulisha kwa mtemi wa kijiji aitwaye Masasa. Katika kijiji waliweza kumjadili Sekai na mtoto wake ingawa ilikuwa vigumu kumkaribisha Sekai katika kijiji chao lakini hatimaye walimruhusu. Mzee Chivero ndiye aliyekuwa mlezi mkuu wa Sekai na mtoto wake.
  1. Maisha mapya ya Sekai
Ujio wa Sekai katika kijiji kile kipya ulikuwa gumzo kijiji chote. Wazee wa kijiji walikutana na kuweza kumjadili mgeni huyo aliyeingai katika kijiji chao. Wazee hao waliongozwa na mtemi Masasa.
Kulikuwa na imani zilizofuatiana juu ya ujio wa Sekai na mtoto wake maana walijiuliza maswali mengi pasipo kupata majibu sahihi. Na hatimaye walifikia tamati na wote walikubaliana kutomfukuza mgeni huyo maana mizimu ya kijijini hapo ilipinga kumfukuza mgeni yeyote atakayeingia kijijini hapo kinyume na hivyo kungepelekea laana kubwa toka kwa mizimu ya hapo kijijini.
Matumaini ya kuishi kwa Sekai na mtoto wake aliyekuwa Zeruzeru yalirejea upya baada ya kukubaliwa na wazee wa kijiji kuishi katika kijiji kile alichofikia.
Sekai aliweza kujengewa makazi yake pamoja na mwanae na kujishughulisha na shughuli zote za uzalishaji kama wanakijiji wengine.

Baadhi ya wanakijiji walimtenga Sekai na mtoto wake hasa upande wa wanawake wenzake. Lakini hili halikuwa tatizo kwake bali yeye alifurahia maisha mapya na yenye matumaini na aliweza kumshukuru sana mzee Chivero kwa usamalia wake wa kumsaidia yeye na mtoto wake ambaye ni Zeruzeru.
  1. Sekai apata rafiki
Sekai alikuwa mwanamke mchapakazi na hodari kama wanawake wengine hapo kijijini. Mzee Chivero alipata msaada mkubwa kutoka kwa Sekai kwa kufanya shughuli za nyumbani kwa mfano, kuandaliwa chakula.
Sekai alikuwa mpweke na mwenye huzuni maana wanawake wenzake walimtenga na mbaya zaidi alipokuwa akitoka shamabani njiani alikuwa akikutana na wanawake wenzake. Wanawake wajawazito hawakupenda kupishana naye na punde walipomuona walijifunika mikono yao usoni au walirudi nyuma ilimradi tu wasikutane uso kwa uso na Sekai. Mzee Chivero alitambua hilo na hivyo alikwenda kuomba msaada wa ufumbuzi wa tatizo hilo kwa mtemi Masasa na ndipo mtemi alimruhusu mzee Chivero amchukue Tendai ili amtambulishe kwa Sekai ili awe rafiki yake.
Tendai alikuwa mke wa mwisho na mdogo wa mtemi Masasa. Mzee Chivero alimtambulisha Tendai kwa Sekai. Hatimaye, Tendai ndiye aliyekuwa rafiki mkubwa wa Sekai na waliweza kushirikiana katika shughuli mbalimbali za kijamii.
Takadini sasa alifikia umri wa kuweza kukaa na hata kumtambua ipasavyo mama yake. Tendo hili lilimuongezea furaha na matumaini makubwa Sekai.
  1. Tukio la ajabu lamtokea Sekai
Siku moja alikuwa akirejea nyumbani toka shambani njiani aliona vijana ambao walikuwa wakirina asali.
Ghafla kundi la nyuki lilimvamia na ndipo Sekai alimtupa mtoto kichakani na yeye alijitosa majini ili kunusuru maisha yake pamoja na mwanae. Sekai alifanikiwa kuokoa maisha yake na ya mtoto pia ingawa walipata maumivu makubwa ya kuumwa na baadhi ya nyuki.
Mzee Chivero alipata taarifa hizo na aliweza kutoa msaada wake kwa kuwatibu na alitumia dawa za mitishamba na hatimaye Sekai na mwanae walirejea katika afya yao ya kawaida kama ilivyokuwa awali.
Lakini kwa Takadini haikuwa hivyo kwani alidhurika sana na aliweza kupata kilema cha maisha katika mguu wake ambacho kilitokana na kutupwa kichakani na mama yake katika harakati za kunusuru maisha yake. Huzuni kubwa ilimjia tena Sekai na aliwaza mengi juu ya mtoto wake. Pia alipatwa na uchungu na alijiuliza maswali mengi kwa kuhisi ameikosea mizimu yao kwa yeye kutoroka kijijini kwake.
Lakini Sekai alijikaza na aliamini kuwa yeye ni shupavu na yote hayo aliwaachia mizimu, hivyo muda mfupi alirejea katika hali yake ya kawaida kama alivyokuwa awali.
  1. Maisha ya Takadini
Takadini alikuwa na furaha kubwa bila kujali hali yake na wakati huo alianza kutambaa kwa kuvuta mguu mbovu wa kushoto. Pia. Takadini alitaabika sana wakati wa mwanga mkali na joto la jua lilimuumiza kiasi ambacho shingo yake ilienea michubuko. Kwa mapenzi ya mzee Chivero, Tendai na mama yake, Takadini alijiona ametimia kwani waliongea naye, wakacheza naye na wakamfanya ajisikie anapendwa na mwenye furaha.
Takadini alitengwa na watoto wenzake na pia walimdharau kwa kumwambia yeye alikuwa ni Sope na tena amelaaniwa.
Mzee Chivero alipokuwa akielekea msituni aliongozana na Takadini huko msituni alimfundisha jinsi ya kufahamu dawa za mitishamba na matumizi yake mbalimbali.
Takadini alionekana kuwa ni mtoto mwelevu mwenye kupenda kufahamu mambo mbalimbali. Siku moja Takadini alihuzunika sana pale alipoambiwa na watoto wenzake kuwa yeye ni Sope na tena amelaaniwa, ndipo kitendo kile kilimfanya Takadini akose raha kabisa. Mzee Chivero na mama yake walimfariji Takadini na ndipo mzee Chivero alimfariji kwa kumwambia, “Mbuyu sio mwembamba na mzuri kama miti mingine, lakini ni imara na unaishi maisha marefu kuliko miti yote msituni na ni mti wenye matumizi makubwa”. Hivyo Takadini alipofikiri akajilinganisha na mti ule kama ulivyotofautiana na miti mengine ndivyo yeye alivyotofautiana na wengine.
Akaongeza kwa kumwambia tena “Hakika wewe ni wa kipekee, na ndiyo maana upo tofauti nao, lakini bado hawajui kuwa wewe ni pekee kiasi gani.
  1. Maisha ya Takadini
Siku moja mzee Chivero anamletea Takadini mbwa ambaye alikuwa ni rafiki sana na Takadini hasa alipokuwa akienda msituni peke yake. Mzee Chivero alitambua hatokuwa na Takadini siku zote maishani hivyo mbwa yule angekuwa mlinzi mkubwa wa Takadini, mbwa huyo aliitwa Shumba.
Takadini alipenda sana kusikiliza hadithi mbalimbali zilizokuwa zikisimuliwa na wazee katika dare kama vile Tsuro mwenye busara. Takadini alipofikisha miaka kumi na tatu hali ya afya ya mzee Chivero ilidhohofu na alianza kukohoa muda wote, ndipo alianza kumuagiza Takadini dawa za kumletea toka msituni na Sekai aliendelea kumtunza vyema.
Takadini alijifunza kutabiri kwa kutumia mifupa na kujua sifa mbalimbali za miti shamba ambayo mzee Chivero alikusanya maishani katika kutibu maradhi mabalimbali.
Katika kijiji hicho kulitokea matukio makubwa mawili, kwanza ni sherehe ya mavuno ambayo iliambatana upigaji wa mbira na pia watu hucheza wakubwa kwa watoto, wanaume kwa wanawake.
Takadini alivutiwa sana na upigaji mbira lakini aliwaza ni nani atakayemfundisha maana alikuwa hana rafiki. Lakini hakukata tamaa ndipo akamueleza mzee Chivero. Mzee Chivero alimahidi kumtafutia mtu atakayemfundisha.
Tukio la pili katika kijiji hicho ni kutokea kwa mvua kubwa na kufariki kwa wazee maarufu kijijini hapo. Alianza kufariki mtemi Masasa ambaye alikuwa kiongozi wa kijiji kile na ndipo akafuata mzee Chivero ambaye alkuwa mganga mashuhuri kijijini hapo.
Wanakijiji wotw walihuzunika sana Sekai na Takadini walihuzunika sana baada ya kuondokewa na mzee Chivero ambaye alikuwa ndio mlezi wao na mwenyeji wao mkuu. Baada ya miezi kadhaa Sekai na mwane Takadini walirejea katika hali ya kawida na kuendelea na shughuli za kila siku.
  1. Maisha ya Takadini baada ya kifo cha mzee Chivero
Ulipita mwezi baada ya kifo cha mzee Chivero, ndipo siku moja mcheza mbira maarufu alipomtembelea Sekai na kumfahamisha juu ya ujio wake pale nyumbani kumfundisha Takadini kupiga mbira. Kwani aliagizwa na mzee Chivero kabla hajafariki. Takadini aliitwa na akaelezwa na baba Kutukwa kuhusu kumfundisha jinsi ya kupiga mbira. Takadini allifurahi sana na muda mfupi alianza mazoezi hatimaye alikuja kuwa hodari wa kupiga mbira.
Mzee Kutukwa alikuwa ni mzee mwenye busara kwani alimpenda sana mtoto yule aliye mpweke na alimsaidia sana kwani siku moja aliwaza kumsaidia Takadini ndipo alimtengenezea mti mzuri ambao ungemsaidia Takadini wakati wa kutembea kwani hapo mwanzo alipata shida sana kwa kutembea kwa kurukaruka.
Takadini alijawa na furaha baada ya kukabidhiwa mti ule na alianza kutembea kwa haraka sana, na huku akiwasalimu rafiki zake njiani, na wao walimshangaa sana.
Furaha na shukrani vilimjia Takadini katika nafsi yake na ndipo alichukua mbira akaanza kupiga huku akiimba wimbo mpya ambao ulimjia kama taswira akilini mwake:

“Nawashukuruni baba zangu, Chivero kwa kunikamilisha, kwa kunipa fruraha kwa kunijaza moyo wangu kwa muziki na amani”.

Sekai alivutiwa sana na wimbo huo uliokuwa mpya masikioni pake hivyo naye aliishukuru mizimu kwa furaha aliyonayo.
  1. Tukio la kusikitisha latokea kijijini
Miezi sita ilipita baada ya Takadini kuanza kupiga mbira. Vijana wote wa kijijini hujishugulisha na uchungaji wa mifugo yao na pindi wawapo machungani huonyeshana ubabe wa kupigana ili kujua nani zaidi.
Ilikuwa ni tofauti na siku zote siku hiyo waliendekeza mchezo wao kama kawaida yao kumbe siku hiyo alitokea simba mkubwa na akamla ng’ombe mmoja ambaye ni maksai. Kitendo hicho kiliwasikitisha sana wanakijiji hivyo walijawa na woga dhidi ya simba huyo.
Wanakijiji wanapanga kuingia msituni ili kumsaka simba huyo na hatimaye wanafanikiwa kumuua simba huyo. Baada ya ushindi huo, wanakijiji wanafanya sherehe kubwa ili kujipongeza kwa ushindi huo.
Takadini alikuwa mmoja kati ya wapigaji mbira katika sherehe hiyo. Lakini baadhi ya watu walikasirishwa na tendo la kumhusisha Takadini ambaye alikuwa ni Sope (zeruzeru) watazamaji na wachezaji siku hiyo walifurahishwa sana na upigaji mbira wa Takadini na wimbo wake ambao watu wote waliupenda.
Baadhi ya wasichana walivutiwa sana na uhodari wa Takadini akiwepo msichana mmoja aitwaye Shingai.
Shangai alitoke kuvutiwa sana na Takadini hivyo alitumia kila mbinu ilimradi awe karibu na Takadini.
Siku moja Shingai aliteka maji mtoni na kumpelekea Sekai nyumbani kwake na ndipo Sekai anastaajabu kwa tendo lile lakini Shingai anathibitisha kwa kumwambia amejitolea tu kwani kwake anaona si vibaya kumsaidia mtu mkubwa.
Hatimye habari zilienea kijiji kizima kuhusu kitendo cha Shingai alichofanya.
Wazazi wa Shingai walichukizwa sana. Wazee wa kijiji nao waliweza kujadili hili na ingawa hawakufikia muafaka wa tukio hilo.
  1. Gumzo kijijini dhidi ya Takadini
Tendai anamtembelea Sekai nyumbani kwake na wanajadili juu ya Takadini na Shingai. Baada ya Shingai kuzuiliwa kutokewenda tena nyumbani kwa Sekai, hivyo Shingai alikuwa mpweke sana na mwenye mawazo juu ya Takadini. Hivyo ndivyo ilivyokuwa hata kwa Takadini kwani alijihisi kukosa amani.
Shingai alipendwa sana na kijana aitwaye Nhamo, lakini Takadin na Nhamo walikuwa maadui toka utotoni.
Ilifanyika tena sherehe nyingine kubwa hapo kijijini maalumu kwa kumkumbuka marehemu mzee Chivero na Takadini alichaguliwa katika ku
piga mbira. Takadini alionyesha umakini wake hasa pale alipoimba wimbo wake mwenyewe wa kumtunza mzee Chivero. Sauti yake ilikuwa nzuri na kila mtu alivutiwa naye na kusahau kama aliyecheza na kuimba ni Sope(zeruzeru). Shingai naye hakuwa mbali, bali naye alikuwepo katika sherehe hiyo pia hata Nhamo alikuwepo akifuatilia nyendo za Shingai na Takadini.
Hatimaye Nhamo aliweka mambo wazi juu ya azma yake ya kumuoa Shingai na alimtuma munyai (mshenga) akatoe taarifa nyumbani kwa akina Shingai lakini Shingai hakuvutiwa na Nhamo bali alivutiwa na Takadini.
Siku moja Nhamo alikwenda nyumbani kwa akina Takadini na akamtahadhalisha aachane na Shingai vinginevyo atampiga. Kitendo hiki cha kitisho kilimnyima raha Takadini lakini alipiga moyo konde.
Chido naye alikuwa msichana ambaye naye alivutiwa Sana na Nhamo hivyo Chido na Shingai alikuwa hawapatani. Swala hili lilimjengea sana hofu Shingai kwani hakupenda kuchangia mume mmoja na Chido. Shingai alitamani awe na ujasiri kama wa Sekai ambapo alipingana na wazee wa kijiji na hata Takadini akakua baada ya kuuawa.
Wakiumizwa na haja ya kuficha hisia zao za kweli, Shingai na Takadini walitafuta mbinu za kuweza kuonana. Tambudzai alikuwa ni rafiki wa Shingai na alikuwa akimsaidia sana Shingai pindi wasichana wenzake walipomsema baada ya yeye kuhisiwa kuwa ana mahusianao na Takadini.
  1. Furaha ya Takadini.
Ulibaki mwezi mmoja kabla ya ndoa kati ya Nhamo na Shingai. Takadini alitumia muda mwingi kujifariji na mbira yake kwa kumkomoa mpenzie. Kabla ya ndoa, mzee maarufu aitwaye Makaure alifariki dunia hivyo wanakijiji walihuzunika sana.
Siku moja katika kibanda chake Takadini alisikia mtu akifungua mlango na alipotahamaki alimuona Shingai akiingia ndani mle katika usiku wa kiza. Shingai alimkaribia Takadini na akavuta gudza na wakajikuta wanafanya tendo la ndoa. Jua lilipochomoza Shingai hakuonekana kwao na walipomtafuta walimkuta kwa akina Takadini.
Familia ya akina Shingai ilimtenga kuanzia siku ile lakini Sekai hakumfukuza Shingai nyumbani kwake. Wazee wa kijiji waliwajadili sana Shingai na Takadini lakini walifikia tamati kwa kusubiri kitakchoendelea.
Nhamo aliamua kumua Chido badala ya Shingai. Chido na Nhamo wakaungana kumchukia Takadini. Chido alimchukia sana Shingai baada ya kujulikana ana mahusiano na Takadini.
Baada ya siku chahe Shingai aligundulika kuwa ni mjamzito. Muda mfupi alijifungua mtoto wa kiume ambaye si Sope(Zeruzeru) tena, bali alikuwa kama watoto wengine. Sekai alijawa na furaha na kujisemea moyoni, “kumbe Takadini ni rijali”.
Tendai alimshukuru sana Sekai na alimwambia kuwa yeye na Takadini wameleta mabadiliko kijijini hapo hasa katika kumdharau mtu aliye na ulemavu kama Takadini. Sekai alimshukuru rafiki yake na alipanga kurejea na familia yake katika kijiji chake cha nyumbani.
Je, taswira hiyo ya mila dhidi ya Masope(mazeruzeru) ingepokelewaje na jamii ya mama yake Takadini pindi watakaporejea?

C. MAUDHUI
DHAMIRA KUU:
Ukombozi wa kiutamaduni
Dhamira kuu katika riwaya hii ni ukombozi wa kiutamaduni.
Mwandishi anaonekana kusukumwa na tatizo la jamii kukumbatia mila na desturi zilizopitwa na wakati.
Katika jamii kuna mila na desturi zimetumika kama chombo cha ukandamizaji. Mila na desuri zimeelezwa kutumika kukandamiza wanawake na watooto katika vipengele vifuatavyo:
  1. Ndoa
  2. Mirathi
  3. Uhai
  4. Maamuzi
  5. Mgawanyo wa kazi
  6. Mgawanyo wa mapato na umilikaji wa mali
  7. Elimu
  8. Utu
Waandishi wengi kama vile Ebrahimu Hussein katika tamthiliya yake ya Kwenye Ukingo wa Thim, Penina Mhando katika pambo, N.k. wamejadili namna baadhi ya mila na desturi zinavyotumika katika ukandamizaji wa wanawake, watoto na walemavu.
Mwandishi wa riwaya hii, anaonesha namna mila na desturi mbaya zinavyotumika kuwakandamiza wanawake na makundi mengine ya wasiojiweza. Mfano wa mila na desturi zinazotishia uhai, haki na maisha ya watoto walemavu kama Takadini, kijana aliyejaliwa akiwa zeruzeru ambaye jamii yake iliazimia kumuua siku ya pili baada ya kuzaliwa kwake. Katika ukuraasa wa 19 mwandishi anasema.
Sekai alimpenda Makwati – siku zote alimpenda . Na sasa anamuacha aamuliwe na wazee kwa sababu ameshindwa kumpatia aina ya mtoto aliyetaka… mtoto huyu asiye na msaada alimtegemea yeye kama tu alitaka aishi. Katika kijiji hiki, kati ya watu wa Makwati, Zeruzeru hak
uwa na nafasi”.
Kauli hii inathibitisha kuwa jamii haikuthamini mtu ambaye alikuwa ni mlemavu. Wazee wa kijiji ndiyo walikuwa wasimamizi wa mila na desturi hizi za kikatili. Takadini kama mlemavu maisha yake yaliokolewa na mama yake ambaye aliamua kuvunja shina na miiko iliyowekwa ili kuangamiza Zeruzeru.
Uonevu wa mila na desturi huakuwalenga watoto tu, bali ukandamizaji uliwagusa pia wanawake katika jamii. Mwandishi anamuonesha Sekai kama mhanga wa mila na desturi zinazokandamiza wanawake. Baada ya kuzaa mtoto aliyekuwa na ulemavu (zeruzeru) na kukataa mwane asiuawe, Sekai naye kifo kilimkabili kwa mujibu wa mila na desturi za kabila lao. Haya yanaweza kuthibitishwa na maelezo ya Makwati akimtahadharisha Sekai, alisema,
Lakini Sekai kama wataamua mtoto auawe, hata nawe utauawa kwa sababu ya kupinga sheria za kale”.
Kauli hii inaonyesha namna wazee walivyotumia mila na desturi ‘katili’ kutoa hukumu kubwa ambayo Mungu pekee angestahili kuitoa na si mwanadamu yeyote. Hukumu ya kukatisha maisha ya binadamu ni ya ukatili. Wazee waliazimia kutekeleza sheria, mila na desturi za kabila lao bila kujali madhara yake.
Je, haitupasi sasa kuleta ukombozi wa kiutamaduni kwa kurekebisha baadhi ya mila na desturi zilizopitwa na wakati? Wakati umefika sasa kwa jamii kuliona hilo. Kuwa tayari kuzifanyia marekebisho baadhi ya mila ambazo zinatuumiza wenyewe. Kwa gharama yoyote ile tunapaswa kutetea haki, uhuru na utu wa watu wote dhidi ya mila na desturi zinazokiuka haki, uhuru na utu wa mtu.
Mwandishi anasema,
Sekai alikwishaamua: lazima aondoke asubuhi itakayofuata.Sekai hakuwahi kutenda jambo kinyume na Makwati wala mila zao, isipokuwa kwa hili, kulilia uhai wa mtoto wake. Uamuzi wake ulikamilika kwa usahihi na ushwari, sifa ambazo hakujua kuwa alikuwa nazo.”
Jamii inapaswa kuwa jasiri kama Sekai aliyeamua kuvunja, sheria zilizokuwa zimepitwa na wakati.
Mwandishi anaonesha pia namna mila na desturi zinavyoingilia hata masuala ya ndoa. Mwanamke alinyimwa haki ya kuchagua mtu anayempenda kuwa mume wake, kama inavyoonekana kwa Shingai. Hata kivyo Binti huyu pia alipigania haki na uhuru wake kwa kumkataa mchumba aliyechaguliwa na wazazi wake. Katika kutetea uhuru na haki yake, Shingai anasema,
Huyu ndiye mtu ninayetaka aniowe. Hakuna aliyeniuliza kama nampenda Nhamo. Wewe na baba mlikuwa na hamu ya kuniozesha katika familia ya Manyamombe hata matakwa yangu hayakusikilizwa. Sasa nimechagua . Nakuomba msamaha wako mama, unaweza ukaniua kama ukitaka, lakini katu kwa Nhamo siendi hata kama angekuwa nami sasa”.(uk118).
Je, ni nani ataleta mabadiliko kama siyo sisi wenyewe tunaoathirika na milahizi mbaya? Shingai anatuonesha njia kuwa ukombozi wowote ule ni lazima tuwe tayari kujitoa mhanga kama alivyofanya Sekai na Shingai ambao walileta mabadiliko katika jamii zao. Tendai anashuhudia hilo kwa kusema.
“….Sekai. Wewe na Takadini mmebadilisha mambo mengi kijijini hapa. Kwa sasa, sifikirii kwamba kuna mtu yeyote atakayekuwa na moyo wa kuharibu watoto wachanga Masope au wenye ulemavu. Ahsante nyingi kwako na Takadini na kwa baba Chivero. Ndiyo hurejea huko baada ya muda mrefu hivi huenda kukawapa funzo kama hili pia…..”(uk.126).
Kwa ujumla mwandishi amejaribu kuonesha baadhi ya mila na desturi zenye walakini katika jamii nyingi za kiafrika na ameonesha njia za kuondoka nazo ili kuleta ukombozi.
Dhamira Ndogondogo
Katika riwaya hii, kuna dhamira mbalimbali ambazo zimeijenga dhamira kuu. Dhamira hizo ni pamoja na hizi:
  1. Mapenzi
  2. Ndoa
  3. Imani potofu
  4. Upendo
  5. Ujasiri
  6. Umoja na mshikamano
  7. Elimu
  8. Nafasi ya mwanake
Dhamira hizi zote zinajenga dhamira kuu ya ukombozi wa kiutamaduni kwa kuonesha sheria, mila, na deturi zinavyogusa dhamira zote hizo.
  1. Mapenzi
Mapenzi ni dhamira ambayo imejadiliwa katika riwaya hii ya Takadini. Mwandishi amejaribu kuonesha kuwa katika jamii kuna aina mbili ya mapenzi. Mapenzi ya dhati na mapenzi yasiyo ya dhati. Mwandishi anaona kuwa mapenzi ya dhati ndiyo humfanya mtu aheshimu wengine, ajali haki na utu wa mtu, ajisikia uhuru na kukwepa kupandikiza chuki na badala yake humfanya ahimize ushirikiano, umoja na upendo.
Katika riwaya hii ya Takadini tunaona mapenzi ya dhati kati ya Takadini na mama yake. Takad
ini na mzee Chivero, Takadini na Shingai, Sekai na Pindai, na Sekai na mzee Chiro.
Mapenzi ya Sekai kwa Takadini (mwanae) yalikuwa ya dhati kwa sababu Sekai alikuwa radhi kufa ilimradi mwanae Takadini asipate madhara. Sekai alimlinda mwanae wakati wote, Sekai alikabiliana na mumewe katika hali ya kumlinda Sekai anasema,
Ni mtoto wangu wa kwanza niliyemsubiri kwa miaka mingi. Siwezi kukubali kumpoteza. La humataki, nirejeshe kwetu au hata msituni, lakini usije kunilazimisha nitengane naye. Nitajitoa mhanga kwa ajili yake”.
Haya ni mapenzi ya dhati ya mama na mtoto wake. Mama alijitoa mhanga kumlinda mwanae katika hali ya hatari. Alijua fika nini kitamkabili mbeleni kwa kufanya mambo kinyume na taratibu za kabila lake.
Mapenzi ya dhati yanajitokeza kati ya Takadini na Shingai. Takadini ni kijana mwenye ulemavu wa aina mbili (mguu na ni zeruzeru) hivyo alitengwa na jamii.
Katikati ya upweke wake ambao umetokana na ulemavu anapumzishwa machungu hayo na binti aitwae Shingai . Shingai alikuwa na mapenzi ya dhati kwa Takadini. Ingawa wazazi wake walimkataza na kumchagulia mchumba, Shingai alikuwa na msimamo na kuelezea wazi hisia zake kwa wazazi wake. Katika hali ya kutetea penzi lake la dhati Shingai anasema,
Huyu ndiye mtu ninayemtaka anioe. Hakuna aliyeniuliza kama nampenda Nhamo. Wewe na baba mlikuwa na hamu ya kuniozesha katika familia ya Mnyamombe hata matakwa yangu hayakusikilizwa. Sasa nimechagua. Nakuomba msamaha wako mama, unaweza ukaniua kama ukitaka, lakini katu kwa Nhamo siendi hata kama angekuwa namI sasa.”(uk118).
Uamuzi huu unadharirisha kuwa mapenzi ya dhati hayachagui rangi, kabila, mali au vitu vingine. Mbali ya kukanwa na wazazi wake Shingai hakubadili msimamo wake. Alitunga mimba na kuzaa mtoto. Shingai anadhihirisha penzi la dhati kwa Takadini.
Mapenzi mengine ya dhati ni kati ya mzee Chivero na Sekai. Wakati wa kutoroka, Sekai anakutana na mzee Chivero na anamweleza mkasa wote uliompata na lengo lake yeye kutoroka. Mzee Chivero anamkaribisha Sekai katika kijiji chake na anamtambulisha kwa Mtemi wao. Mzee Chivero ndiye aliyekuwa, mlezi mkuu wa Sekai na mtoto wake hadi kifo kilipomchukua. Hivyo inaonesha wazi kuwa mzee Chivero alikuwa mkarimu na mpole kwa wageni na hivyo alikuwa na mapenzi ya dhati.
Mapenzi kati ya mzee Chivero na Takadini vilevile yalikuwa ya dhati. Mzee Chivero alimpenda sanaTakaini kwani alimfundisha mambo mbalimbali kama vile uwindaji, alimfundisha jinsi ya kufahamu dawa za mitishamba na matumizi yake mbalimbali. Kila wakati Takadini alipokuwa na huzuni alifarijiwa na mzee Chivero.
Vilevile mapenzi kati ya Sekai na Pindai yalikuwa ni ya kweli. Pindai alikuwa mke mwenza wa Sekai na alimpenda sana kuliko wake wenzake ambao kila wakati wakilimsengenya Sekai kwa sababu ya kutopata mtoto. Lakini wakati wote Pindai alifariji Sekai kutokana na kusengenywa na wake wenza.
Mapenzi mengine ya kweli ya dhati ni kati ya Sekai na Tendai. alikuwa mke wa mwisho na mdogo wa Mtemi Masasa. Tendai ndiye alikuwa rafiki mkubwa wa Sekai na aliweza kushirikiana katika shughuli mbalimbali za kijamii.
Kwa upande wa mapenzi ya oungo yasiyo ya dhati nayo yamejadiliwa katika riwaya hii, kwanza mapenzi ya uongo ni kati yam zee Makwati kwa mtoto wake Takadini. Mzee Makwati alikasirishwa na kitendo cha kuzaliwa takadini akiwa Zeruzeru, kutokana na kitendo hicho mzee Makwati alifuata mila na alitaka Takadini auawe kwani aliona kuzaliwa kwake ni kama kuleta balaa katika familia yake, lakini mama yake Sekai alitoroka na mtoto ili asiuawe.
Mapenzi ya uongo ni kati ya mzee Makwati na Sekai baada ya kujifungua mtoto Zeruzeru. Mzee Makwati alikasirishwa kwa kuona mtoto yule na alimshutumu mkewe kuwa alitembea na wanaume wengine hivyo alivunja mila na desturi zao. Sekai aliumizwa sana na tuhuma hizo maana alijiona hana maana tena mbele ya mumewe na alijihisi ametelekezwa zaidi wakati huo.Kutokana na kitendo hicho cha kutelekezwa na mume wake sekai aliamua kutoroka.
Mapenzi mengine ya uongo ni kati ya Dadirai na Rumbiozai kwa Sekai, hawa walikuwa ni wake wenza wa Sekai na waliishi maisha ya kumsengenya Sekai kila wakati. Hawa hawa kuwa na mapenzi ya kweli kwa Sekai, kwani waliishi kwa kumbaguana Sekai walikuwa na wivu naye na matokeo yake kukawa na mvurugano wa kifamilia.
  1. Ndoa
Ndoa ni makubaliano kati ya watu wawili wapendanao ambao wameamua kuishi kama mume na mke. Maamuzi ya juu ya nani awe mume au mke ni juu ya wale wapendanao. Mila na desturi zimeingilia ndoa za watu katika jamii madhara yake yamekuwa makubwa: Ndoa zimevunjika na hata kukosekana kwa amani.
Katika riwaya hii , Shingai alilazimishwa kuolewa na Nhamo. Kitendo hiki hakikumfurahisha Shingai. Alisema
Ama! siyo kama ninamchukia Nhamo, la hasha. Isipokuwa sidhani kama nitakuwa na furaha kuishi naye.” (uk.110).
Ingawa mila na desturi ziliwabana watoto wa kike kuwa na uhuru lakini ukweli ni kwamba mila hizo zilisababisha ndoa nyingi kutokuwa na furaha. Shingai anasisitiza.
Sikumwambai kufanya hivyo na simtaki. Nataka waniache peke yangu ili naimue mwenyewe…..” (uk115)
Pia mwandishi wa riwaya hii amegusa suala la ndoa za mitala. Mwandishi ameonesha kuwa ndoa za mitala ni desturi ambayo jamii inapaswa kuachana nayo. Mwandishi ameonesha namana ndoa za mitala zinavyochangia kuleta mifarakano katika familia. Mfano mzuri ni namna wake zake Makwati walivyokuwa wakiishi kwa kusengenyana na uadui mkubwa ulizuka miongoni mwao. Haya yanajitokeza (uk 1- 20). Katika (uk.3) Pindai anasema,
Si ajabu wale wawili wanahofu utapata mtoto wa kiume…. Wanaamini kuwa Makwati atahamishia mapenzi na uangalizi kwa mtoto huyo. Pia, mume wetu atazidisha mapenzi kwako. Aidha wana imani kwamba umepa dawa Makwati ili akupende wewe zaidi ya mwingine.”
Makwati alikuwa na wake wanne ambao walioishi katika maisha ya uhasama sana. Walitukanana na kusingizia mambo mabaya kama uchawi. Kimsingi, penzi haligawiki. Wanajamii wanapaswa kuachana na mila hiyo mbaya ya kuishi katika ndoa inayohusisha mke zaidi mmoja.
  1. Dhana potofu
Katika jamii kumekuwa na hali ya watu kuamini vitu ambavyo havina msingi. Watu wamekuwa wakitelekeza walemavu wa viungo vya mwili, Zeruzeru na hata mapacha kwa kuamini kuwa miungu yao isingefurahia kuwaona watoto hao wenye ulemavu katika jamii. Mwandishi wa riwaya hii hakufumbia macho tatizo hili, amelizungumzia kwa kina na kuwaonyesha njia kuwa mambo ambayo walidhani kuwa yamewezekana. Ziki ni mfano wa watu ambao wamekuwa na dhana potofu maishani mwao. Sekai na Takadini (Zeruzeru) wanapokaribishwa katika kijiji cha watu wa Masasa, Ziki alipinga kuwepo kwao hapo. Anasema,
Sote tunajua mila za mababu zetu katika kila koo na kijiji. Watoto kama huyu lazima wauawe, wenye ulemavu lazima wauawe, na hata pacha mmoja lazima auawe”.
Hii ni kauli ya Ziki ambayee alirejea mila na desturi potofu kuhalalisha dhana potofu alizonazo dhidi ya walemavu. Huyu si mtu ambaye ana dhana potofu, wapo wengi sana. Katika riwaya hii, wapo wazee wengine kama Mapunzure ambaye katika ukurasa 35 alisisitiza, Mtoto lazima auawe.”Pia kama mzee Manyamombe ni mmoja wa watu wenye imani potofu juu ya watoto walemavu.
Kuna dhana potofu pia kuhusu jinsia ya watoto. Wazazi wengi wamekuwa na upendeleo zaidi kwa watoto wa kiume kama ilivyo kwa Makwata na wake zake.
Sekai anapopata ujauzito anatamani mumewe kuwa huenda ujauzito alionao ni wa mtoto wa kike. Makwati aling’aka,
unasemaje we mwanamke?… Hapa tayari tuna idadi kubwa ya wanawake. Mimi nanyong’onyea kwa kuomba mtoto wa kiume.”
Kila mtoto anayezaliwa ana haki ya kupendwa bila kujali jinsia yake.
Dhana potofu katika ni tatizo linalopaswa kuondolewa kwa kutoa elimu sahihi katika jamii ili kuepuka matatizo yasitokee kama mzee Chivero na mtemi Masasa walivyofanya kwa watu wao.
  1. Nafasi ya mwanamke katika jamii na ujinsia
Ujinsia ni majukumu ya kijamii ambayo hupewa mwanaume au mwanamke kwa kuangalia mahusiano ya mtu mume na mtu mke. Ni wajibu wa mume na mke katika jamii.
Katika jamii nyingi kiafrika kumekuwa na matatizo ya jinsia kama vile kuozesha kuwa watoto katika umri mdogo na kulazimishwa kuolewa au bila ridhaa, maamuzi yote yanayohusu jamii na familia hufanywa na wanaume, watoto wa kike wamekuwa hawapewi thamani sawa na watoto wa kiume na suala zima la malezi amekuwa akiachiwa mama peke yake.
Katika riwaya hii, mwandishi ameonesha matatizo ya kijinsia. Kwa mfano, Tendai alilzaimshwa kuolewa na mtemi Masasa na alikuwa na umri mdogo. Sekai anapomuuliza Tendai kama alimpenda mzee Masasa, Tendai alijibu,
Ni heshima kuwa mke wa mtemi mwenye nguvu kama Masasa. Lakini namchukulia kama baba yangu kuliko mume wangu”…(uk.47)
Kauli hii inathibitisha kuwa Tendai hakufurahia kuolewa na mume mwenye umri mkubwa sawa na baba yake. Hii ni kasoro kubwa sana katika suala zima la ndoa. Tendai anaendelea kusema,
Wake wenzangu ni kama mama zangu. Siku zote wananitazama mimi, wananikaripia, na mabinti zao ambao ni wa umri wangu hunicheka kwa dharau kila wanitazamapo…” (uk.47)
Mahusisano ya kijinsia katika jamii yamekuwa katika hali ya kukandamiza zaidi, mwanamke na kumpendelea mwanaume. Katika riwaya hii, mwandishi ametuonyesha tatizo jingine la kijinsia kuwa ndoa za mitala. Ka
tika suala zima la ndoa mitala tunaona mwanaume anapewa fursa ya kuoa mke zaidi ya mmoja. Fursa hiyo haionekani kwa mwanamke. Sababu kubwa inaonekana kuwa mwanamke ni kama chombo cha starehe. Kwa mfano Makwati alikuwa na wake wa nne. Mtemi Masasa alikuwa na wake wengi pia. Hapa mwanaume ndiye mwenye nguvu zaidi.
Kuhusu nafasi ya mwanamke mwandishi amemuonyesha mwanamke kama mzazi na mlezi wa watoto na familia kwa ujumla. Kwa mfano, Sekai ni mama mzazi wa Takadini. Alimlea na kumlinda wakati wote mpaka alipopata mke (Shingai). Mashangai alimzaa Shingai na kumlea wakati wote. Kazi ya kulea ilionekana ni ya mwanamke na si mwanaume. Mashangai anasema,
Shingai sitakuita mwanangu tena, umefanya kitu gani hiki? Hivi ndivyo bibi yako na tete wako walivyokufundisha?…(uk118).
Kauli ya mama mzazi wa Shingai inathibitisha kuwa malezi ya mtoto waliachiwa akina mama, mama wazazi, Shangazi na bibi. Haya si mawazo ya wanawake kuona ni jukumu lao tu, pia hata wanaume walikuwa na dhana hiyo hiyo. Mfano, Baba yake Shingai alimhoji kewe kuhusu malezi ya Shingai kwa kusema,
Hukumfundisha mwanao maana ya tendo hilo, we?…(uk96)
Mwanake amechorwa pia kama mwanamapinduzi. Haya yanaweza kuthibitishwa na wanawake wawili ambao ni Sekai na Shingai. Ni wanawake walioleta mabadiliko katika jamii kwa mfano, Sekai na mwanamke wa kwanza kuvunja sheria za mila na desturi za jamii yake kwa kukataa Takadini(Zeruzeru) asiuawe na akamlinda wakati wote.na alileta mapinduzi akiwa uhamishoni. Rafiki yake Tundai anasema,
Kwa sasa ,sifikiri kwamba kuna mtu yeyote atakayekuwa na moyo wa kuharibu watoto wachanga, Masope au wenye ulemavu…”
Shinga naye anaonekana ni mwanamapinduzi kwa kukataa kuchaguliwa mtu wa kumwoa. Aliamaini kuwa ndoa ya kweli inahusisha watu wawili waliopendana na ambao wamechaguana. Shingai anasema.
Amai, siyo kama ninamchukia Nhamo la hasha. Isipokuwa sidhani kama nitakuwa na furaha kuishi naye”(uk.110)
Anaendela kusema,
Huyu ndiye mtu ninayetaka anioe. Hakuna aliyeniuliza kama nampenda Nhamo… lakini katu kwa Nhamo siendi hata kama angekuwa name sasa”…118
Shingai alisimamia msimamo wake na hata akaamua kuolewa na Takadini na kupata mtoto ambaye hakuwa Sope.
Kwa ujumla, matatizo ya kijinsia yanachangiwa sana na athari za utamaduni (mila na desturi) katika mfumo wa maisha ya jamii. Jamii kuongozwa kwa mfumo unaoegemea jinsia moja ndiyo chanzo cha ukandamizaji wa kijinsia. Jamii zinazofuata mfumo dume, huwa na mila zinazokandamiza wanawake zaidi. Ukombozi wa kiutamaduni utaleta usawa wa kijinsia katika jamii.
  1. Umoja na mshikamano
Umoja ni ile hali ya kuwa pamoja : ushirikiano na mshikamano ni ile hali ya watu kuwa na msimamo na ushirikaino wa karibu katika kutimiza azima Fulani.
Mwandishi wa riwaya hii ameonesha mbinu mojawapo katika kupambana na mila na desturi potofu ni kwa jamii kuwa na umoja na mshikamano. Umoja na mshikamano ni silaha katika mapambano haya. Mshikamano mzuri alionesha mzee Chivero, Tendai, mtemi Masasa ulisaidia kumlinda Takadini dhidi ya wanyanyapaa na hatari ya kupoteza maisha. umoja na mshikamano uliendelea kukua zaidi pale Shingai alipoamua naye kuonesha msimao kwa kukataa kufuatia mila na desturi zilizowabagua walemavu, kuwalazimisha wanawake kuolewa kwa nguvu na hivyo kuamua kuolewa na Takadini ambaye alikuwa ni mlemavu wa mguu na pia alikuwa zeruzeru.
Katika hali ya ushindi dhidi ya mila potofu, mzee Makuru anasema,
Nilimwambia hivyo….. Sasa tunajua ni kipi ambacho mizimu yetu haikuruhusu kutafuta, Sope hawezi kuzaa Sope! Naamini tutajifunza somo hili, fuvu la nyani limekuwa kijiko kwa mlo wa mahindi: vizazi vijavyo vitatushukuru kwa kile tulichokifanya hapa kijijini.”
Katika mapambano yote yote yale, umoja na mshikamano husaidia sana katika kupata ushindi. Wahenga walisema umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Umoja na mshikamano wa Shingai, Pindai, Chivero, Masasa, Sekai Takadini, Makaru na Tendai ulisaidia kuleta mabadiliko makubwa ya kiutamaduni katika jamii yao.
  1. Ujasiri
Hii ni hali ya kukabili jambo bila ya hofu, uhodari, ushujaaa. Katika riwaya hii ya Takadini mwandishi ameonesha ujasiri kama mbinu muhimu katika ukombozi wa kiutamaduni. Pengine ujasiri siyo mbinu inayotumika katika ukombozi wa kiutamaduni tu, bali ni mbinu ambayo imetumika katika aina zote za ukombozi. Mathalani katika riwaya hii tunakutana na Sekai, mwanamke anayeamua kupambana na mila na desturi ambazo ziliwakandamiza wanawake. Baada ya kumzaa Takadini aliamua kumtorosha mwanawe ili asiuawe. Alimkabili mumewe kuwa alitaka kumuona mwanawe akiwa hai. Na hata anapokuwa uhamishoni.
Shingai ni mwanamke mwingine ambaye alionesha ujasiri mkubwa katika harakati za kujikomboa katika makucha ya mila na desturi zilizokuwa zikiwakandamiza wanawake na watoto. Shingai aliamua kuolewa na Takadini (Kijana mlemavu) na kupuuza uchaguzi wa wazazi wake kwa kuwa aolewe na Nhamo. Kwa ujasiri kabisa Shingai anasema,
Huyu ndiye mtu ninayetaka anioe. Hakuna aliyeniuliza kama nampenda Nhamo. Wewe na baba mlikuwa na hamu ya kuniozesha katika familia ya Manyamombe hata matakwa yangu hayakusikilizwa…. Sasa nimechagua.”
Shingai aliendelea nma ujasiri wake huohuo hat baada ya baba yake kutoa kauli za kumkana kuwa mwanae kwa sababu ya kuolewa na Sope (zeruzeru).
Ujasiri ni nguzo muhimu sana katika mapambano dhidi ya mila na desturi potofu katika jamii. Ni lazima tuondoe hofu na woga ili tubadili hali ya ukandamizaji na uonevu ndani ya jamii kwa kunyoshea vidole mila mbaya. Kwa ujumla, malezi ya waatoto ni jukumu la wazazi wote. Mtoto ambaye helelewa vyema na baba na mama ndiye huwa na tabia bora. Jamii inapaswa kutambua kuwa malezi ya baba na mama ni haki ya mtoto, mila ambazo haziendaini na malexi bora hatuna budi kuachana naazo.
  1. Malezi ya watoto
Malezi ni makuzi ya watoto. Ni njia watumiayo wazazi katika ukuzaji wa mtoto kwa kutarajia kufuata tabia na mwenendo unaostahiki.
Malezi ya watoto yanapaswa kusimamiwa na wazazi wote wawili. Baba na mama wanapaswa kushirikiana kwa pamoja katika kulea watoto wote ili watoto wawe na tabia njema. Mila na desturi katika jamii zinazofuata
mfumo dume zinakuwa zikaachwa wanawake peke yao kuwa ndiyo walezi wa watoto. Wanawake ndiyo wanawajibika na malezi ya watoto kwa wanaume zao. Mfano mzuri tunaweza kuupata katika riwaya hii ya Takadini.
Malezi anayopa Shingai ni mama, bibi na shangazi. Baba yake Shingai mzee Nhariswa anamwajibisha mkewe kwa kumpiga kwa sababu Shingai anaonekana kutofuata mila na desturi katika ukurasa wa 119 mzee Nhariswa ansema
umefanya nini sasa wewe mwanamke? Tangu mwanao alipopeleka maji kwa Sekai ungefuatilia kujua anachokifanya …. Uliona dalili, kwa nini hukutafuta dawa…”
Mwandishi anasema kuwa Nhariswa alimpiga mkewe kichwani na usoni mara kadhaa, lakini mkewe hakuweza kujibu. Kitendo hiki kinadhihirisha walakini wa baadhi ya mila na desturi kuhusu suala zima la malezi katika kajamii.
Hivi ndiyo bibi yako na tete wako walivyokufundisha?” (uk118)
Mama huyu naye anaona malezi ya watoto yapo mikononi mwa wanawake na si jukumu la wazazi wote.
“….Mume wangu unasemaje? Kama mtoto wetu ni sope, nitahuzunika sana, lakini nina uhakika atampata wa kumpenda kama nilivyokupenda wewe. Acha kuwa na shaka nimembema mimi na ninaelewa atakuwa kama watoto wengine. Njoo mume wangu tulale sasa.”

Mapenzi ya dhati ni muhimu sana katika ukombozi wowote ule katika jamii.ukombozi wa kitamaduni unawezekana kama kweli watu watakua na mapenzi ya dhati.
Ujumbe
Mwandishi wa riwaya hii anatoa ujumbe ufuatao kwa jamii:
  1. Walemavu wana haki ya kuishi sawa na watu wasio kuwa na walemavu.
  2. Malezi ya watoto yanapaswa kuwa kusimamiwa na wazazi wote wawili ili kujenga jamii inayoheshimika.
  3. Ndoa ni maamuzi ya watu wawili wapendanao na hayapaswi kuingiliwa na mtu yeyote.
  4. Ujasiri, umoja na mshikamano ni mbinu muhimu sana katika ukombozi wa kiutamaduni.
  5. Jamii inapaswa kuachana na mila na desturi potofu ili kuondoa ukandamizaji na unyanyapaa kwa watu wenye ulemavu.
Mtazamo wa Mwandishi
Mwandishi wa riwaya ya Takadini anaoneka kuwa na mtazamo wa kiyakinifu.
Mwandishi anachukulia matatizo yanayotokana na mila na desturi kuwa yanaweza kutatuliwa na watu wenyewe kwa kuchukua hatua za makusudi kabisa katika kujikomboa kiutamadunio kama anavyofanya Sekai, Shingai, Masasa na mzee Chivero. Mwandishi ameweza kuonyesha waziwazi matatizo hayo ya kiutamaduni kuwa ni ukandamizaji wa kijinsia, uonevu kwa walemavu, n.k. Mwandishi pia ameonesha njia za kujokomboa kiutamaduni kuwa ni umoja, mshikamano, elimu na ujasiri.
Kwa ujumla mwandishi ameainisha matatizo yote ya kiutamaduni na kuweza kuonesha masuluhisho ya matatizo haya, hivyo mwandishi anamtazamo wa kiyakinifu.
Msimamo wa mwandishi
Mwandishi ana msimamo wa kimapinduzi kwani ameeleza udhaifu wa baadhi ya mila na desturi zetu. Mwandishi ameonesha madhara ya kuendela kukumbatia mila hizo na akaonyesha hoja ya kufanaya mabadiliko ya badhii ya mila hizo ili kuleta uhuru, haki, usawa na kutahmini utu wa watu wote.
Falsafa ya Mwandishi
Mwandishi anaelekea kuamini kuwa binadamu wote ni sawa hata kama kuna tofauti za kimaumbile. Kila binadamu ana haki ya kuishi. Kwa ujumla mwandishi ni muumini wa haki na usawa.
Migogoro
Katika riwaya hii kumejitokeza migogoro mingi ambayo imetokana na mgogoro wa kiutamaduni.
Mgogoro wa kwanza: Mgogoro wa kiutamaduni kati ya Mkwati na Sekai. Mgogoro huu ulizuka mara bada ya Sekei kuzaa mtoto ambaye ni Sope (Zeruzeru). Kutokana na mila na desturi, mtoto ana ulemavu wowote ule alipaswa kuuawa hivyo Takadini alipaswa kuuawa siku ileile aliyozaliwa. Suala la kuuawa kwa Takadini hakuliafiki Sekai na hivyo kulipinga kwa nguvu zote.
Suluhisho la mgogoro huu ni kwamba Sekai alitoroka na kuishi uhamishoni hadi Takadini alipokua na kuoa na kupata mtoto wa kiume ambaye si sope ndipo aliporudi kijijini kwao.
Mgogoro wa pili : Ni kati ya Shingai na wazazi wake. Wazazi wa Shingai walimchagulia mume wa kumuoa Shingai. Kijana aliyependekezwa aliitwa Nhamo. Jambo hili halikumfurahisha Shingai hivyo alikataa kuolewa na Nhamo na hivyo kufanya wazazi wake kukasirishwa sana kiasi cha kumueleza kuwa asiwatambue kama ni wazazi wake.
Suluhisho la mgogoro huu ni kwamba Shingai aliamua kutorokea kwa Takadini (kijana aliyempenda sana) na kuolewa na Takadini.
Mgogoro wa tatu: Ni wa kinafsia ambao unajitokeza kwa Tendai. Tendai aliozwa kwa mzee Masasa ambaye alikuwa na umri wa baba yake na wakewenza walikuwa umri wa mama yake na mabinti wa Mtemi Masasa walikuwa umri sawa na Tendai. Tendai alishindwa amuite mume wake au baba yake, alishindwa awaite wake wenza au mama zake. Hakuwa amani moyoni. Alikuwa katika hali ya upweke mno.
Suluhisho la mgogoro huu ni kumtafuta rafiki ambaye ni Sekai ili wasaidiane mambo mbalimbali.
Mgogoro wa nne: Ni mgogoro wa kijamii. Mgogoro huu ulitokea kati ya Shingai na Chido. Mgogoro huu ulimhusisha Nhamo kwani Chido alidhani Shingai atolewa na Nhamo na kumfanya awe mkemwenza. Mgogoro ulifanya wanawake hawa wawili watupiane maneno au vijembe.
Mgogoro huu ulisuluhishwa kwa Shingai kueleza msimamo wake wa kutomtaka Nhamo awe mme wake.
Pia Shingai alipoolewa na kuzaa na Takadini ilisaidia kupunguza uhasama huo.
Mgogoro mwingine ni wa kijamii: Huu ni mgogoro wa tano ambao unahusisha Takadini na Nhamo. Nhamo alikuwa ni mgomvi, mbaguzi jambo ambalo alilifanya kwa Takadini. Uhasama zaidi uliongezeka pale Shingai alionesha mapenzi Kwa Takadini Na kumkataa Nhamo. Hakuna suluhisho linalotolewa katika mgogoro huu.
FANI
  1. Muundo
Katika riwaya hii ya Takadini mwandishi ametumia muundo wa msago (moja kwa moja). Visa na matukio katika riwaya hii vilipangwa kwa mfululizo wa moja kwa moja na kazi nzima ina jumla ya sura kumi na tatu. Kwa ujumla muundo wa riwaya hii ni wa moja kwa moja kwani mwandishi anatuonesha namna Sekai alivyopata mimba, akazaa mtoto wa kiume ambaye ni sope(Zeruzeru), kisha anatoroka kwenda kuishi, uhamishoni, maisha ya Sekai uhamishoni, Takadini anakua na kupata mke aitwae Shingai na mwisho tunaona kijijini kwao.
  1. Mtindo
Mwandishi ametumia mtindo wa masimulizi katika riwaya yake. Sehemu kubwa mwandishi amehadidhia mwenyewe kuhusu maisha ya Sekai na Takadini.
Vile vile kuna matumzi ya dayolojia katika sehemu chache. Mwandishi ametumia dayolojia kuonesha uahalisi wa kauli za wahusika wake. Mfano Dayolojia imetumika katika (uk.1)
“Je, Na yule mbuzi wako uliopewa Na baba Makwati, amekupatia watoto wangapi?”
“Tangu nimpate ni miaka miwili tu na tayari ana watoto wawili nabado anatarajia mwingine”.
Haya ni majibizano kaati ya Dirai na Rumbidzai.
Nafasi zote tatu zimetumika. Nafasi ya tatu umoja ndiyo imetalawa katika sehemu kubwa ya riwaya. Kwa mfano:
  • Nafasi ya I ——- “Ndiyo, Pindai, anaogopa……” – (uk.3)
  • Nafasi ya II —– “Unasemaje wewe mwanamke?’’’ (uk.4)
  • Nafasi ya III —— “Sekai alipofumbua macho yake……” (uk.5)
Kuna matumizi ya tanzu nyingine ndani ya riwaya. Mwandishi ametumia nyimbo. Kaatika ukurasa wa pili Rumbidzai aliimba,
“Mashamba yote yamelimwa
Mbegu nazo zimepandwa
Zimechipua na kumea,
Sisi watatu tumepata mavuno yetu;
Mheshimiwa wetu amemiliki mavuno
Kwa mikono yake halisi
Kutoka mashamba yetu yote
Lakini ni kipi alichoambulia
Kutoka ardhi ile isiyomea kitu?…”
Nyimbo nyingine zinajitokeza (uk34, 57, na 90)
Matumizi ya monolojia yamejitokeza pia katika riwaya hii: Mfano wa monolojia:
“Hatimaye!” Sekai alijinong’oneza peke yake.
“Mababu zangu wamenitimizia ombi langu kuu. Sasa wake wenzangu wataniheshimu kama mke wa kwanza. Hata wakwe zangu watakoma kumwambai mume wangu anirejeshe kwetu. Nina hakika ya kijifungua mtotot wa kiume….” (uk1)
Mwandishi pia ametumia mbinu ya hadithi ndani ya riwaya. Mbinu hii imejitokeza katika uk. 82 -84. Kwa ujumla, mwandishi amesheheneza mbinu mbalimbali za kimtindo katika kazi yake.
Matumizi ya Lugha
Lugha iliyotumika inaeleweka kwa wasomaji kuwa wengi. Mwandishi ametumia tamathali za semi, misemo na mbinu nyingine za kisanaa.
a) Misemo na Nahau
Katika riwaya hii kuna matumizi ya misemo na nahau mbalimbali. Misemo na nahau zimetumia kupamba lugha na pia kuonesha uzito wa ujumbe uliokusudiwa.
Kwa mfano:
Lakini mbwa huyu amepoteza meno yake yote”. (uk31).
Hii ni nahau zenye maana ya mtu kutoakuwa rijali tena. Mifano ya misemo ni:
Habari njema huchechemea kwa mguu mmoja, lakini mbaya hukimbia kama sungura.” (uk.15).
Msemo huu una maana ya kuwa habari nzuri hazienei haraka lakini zile mbaya huenea haraka sana. Mifano mingine ya misemo ni:
“Pokea upewacho”…(uk10)
“…Maisha ni matamu”..(uk83)
“Kanga hawezi kutua juu ya bua la mtama…..(101).
“Mume ni kiungo kwa mwanamke.”.(110).
b) Tamathali za Semi
Tashibihi:
Mwandishi amewez
a kulinganisha vitu kwa kutumia vuinganishi kama vile: kama,mfano wa, sawa na, nk
Kwa mfano:
  • Giza jepesi tu lilibaki ukutani kama mgeni asiyekaribishwa na asiyetaka kuondoka.(uk…5).
  • Muda huenda polepole sana mithili ya mwendo wa kakakuona. (uk. 6)
  • Mwanzo maumivu hayo yalitulizana sawa na mwisho wa sentensi ndefu. (uk.6).
  • Mtoto alionekana mweupe sana na funza mkubwa (uk. 16)
Tashihisi
katika riwaya hii ya Takadini mwandishi amevipatia vitu sifa walizonazo watu. Kwa mfano:
  • Ndege mbalilmbali wakiimba kukaribisha siku mpya. (uk. 5)
  • Ubongo wake ulioathirika kwa mawazo uliufukuza usingizi. (uk. 17)
  • Fikra zilizopingana zilijichomeka katika nafsi yake(uk. 17)
  • Miaka mingi iliyomchakaza iliufanya uso uwe sawa na mlima uliomomonyoka ardhi. (uk… 20)
Mubaalagha:
Kuna hali ya utiaji chumvi au chuku nyingi katika masimulizi ndani ya riwaya ya Takadini.
“Mtemi Masasa na wenzake walimtazama Sekai, mcho yao yakipiga mahesabu. Kila mmoja aliridhika naye – tangu monifu nyuma ya miguu yake, mapaja yaliyojaa na hata matiti yake ya duara yaliyojaa maziwa”.(uk.37).
Je, ni kweli wanaume wote waliokuwepo walipiga mahesabu sawa kuhusu Sekai? Mwandishi ametia chumvi kuonesha mvuto tu wa Sekai.
Ritifaa:
Tamathali hii imetumiwa na baadhi ya wahusika kwa kuzungumza nakitu au mtu ambaye husikika katika fikra.
Kwa mfano: Sekai anasoma;
“Hatimaye! Mababu zangu wamenitimizia ombi langu kuu….”(uk.1).

pia katika ukurasa wa 107 manyamombe anasema,

“…Njoo,mpendwa Chivero,umezurura milimani na msituni kwa muda mrefu…
Tusamehe kwa kukuacha mbalimbali …. Njoo rejea nyumbani…. Kunywa pombe hii ….”
Wahusika wote wawili ( Sekai na Manyamombe) walizungumza na watu ambao hawaonekani. Mbinu hii ndiyo tunayoiita Ritifaa.
Dhihaka
Kuna matumzi ya tamathali zenye kunesha dharau na yenye lengo la kumweka mtu katika hali duni kupita kiasi, lakini kwa mbinu ya mafumbo.
Kwa mfano:
  • Naamini alichobeba ni mtoto halisi, siyo dubwasha.” Haya maneno yalimlenga Sekai kwa kuwa siku zote waliamini hazai.(uk.2).
  • Ha! Yawezekana hana tatizo lolote lile, labda alikunywa maziwa mengi wakati wa ujauzito….”
Kauli hii ilitolewa kwa Sekai baada ya kubaini kuwa amezaa mtoto Sope.
Tafsida:
Mwandishi kwa kiasi kikubwa amezingatia utamaduni wa lugha ya Kiswahili. Ameweza kutumia maneno ambayo yanaficha ukali wa maneno. Hakutumia lugha ya matusi. Kwa mfano:
  • Akamshambaulia hata sehemu zake za siri. (uk.83)
  • “A kajivuta karibu zaidi naye, chini ya gudza. Hawakuzungumza, wakafanya kile ambacho kilitokea kwa asili ya maumbile. Wakakata kiu ya hisia zilizowavuta pamoja miezi mingi”. (uk.117)
  • “Walifanya tena tendo la ndoa, …”(uk. 117)
c) Mbinu nyingine za kisanaa
i) Takriri: Kuna baadhi ya silabi, maneno na sentensi zimejirudia kwa lengo la kuonesha msisistizo.
Kwa mfano takriri imejitokeza katika (uk.62)
Pale Nhamo anaposema,
  • Wewe ni Sope, sope, sope”
  • “Najua, najaua” (uk.79)
ii) Mdokezo:
Kuna hali ya kutatiza maneno bila kukamilisha sentensi katika riwaya hii.
Kwa mfano:
  • “Siku moja sijui lini …. Lakini hivi” (uk.75)
  • “Sukuma mara moja tena…” (uk.125)
  • Mtu mzima kama watu wengine na amea…..?
Nidaa:
Kuna kauli ambazo zinaonyesha kushangazwa kwa jambo Fulani. Kwa mfano:
“Ah, Ha! – (uk.118)
“Kumbe maisha ni matamu!” (uk83)
Tashititi:
Hi ni mbinu ya kuuliza swali kwa jambo ambalo anafahamu jibu lake.
Kwa mfano:
“Huenda atakuwa wa kike”. Sekai alisema bila dhamira kubwa.
“Unasemaje we mwanamke? Makwati aliongea kwa sauti kali.
Swali analouliza makwati tayari jibu lake analo.
Wahusika
A.Takadini
  • Huyu ndiye mhusika mkuu wa riwaya hii.
  • Ni mtoto wa kwanza wa Sekai.
  • Ni mlemavu wa ngozi (Zeruzeru) na ana tatizo la mguu.
Kijana wa kiume.
  • Ni mchapakazi na mtu anayependa kujifunza.
  • Ni mwenye huruma.
  • Ni mtiifu.
  • Ni jasiri.
  • Ni mwanamapinduzi.
  • Ni mhanga wa mila na desturi mbaya zinazobagua walemavu.
  • Anafaa kuigwa na jamii.
B:Sekai
  • Huyu ni mhusika mkuu mwingine.
  • Ni mke wa kwanza wa Makwati.
  • Ni mwanake mchapakazi.
  • Ni mhanga wa mila na desturi zilizopitwa na wakti.
  • Ni mwanamapinduzi.
  • Ni mama mzazi wa Takadini.
  • Ni jasiri.
  • Ni mwenye huruma.
  • Ni mwenye busara.
  • Ni mvumilivu.
  • Ni mnynyekevu.
  • Ni mchapakazi.
  • Ni mpole.
  • Ni mama mzazi na mlezi mzuri wa familia
  • Ni mama mwenye upendo.
  • Ni mpishi mzuri wa chakula.
  • Anafaa kuigwa na jamii
C: Makwati
Anafaa kuigwa na jamii.
Ni mkale.
Ni mwoga.
Ana upendo kwa mkewe.
Ni mume mwenye wake wanne.
Ni baba mzazi wa Takadini.
Ni mume wa Sekai.

D:Chivero
  • Ni mzee wa makamo.
  • Ni mganga wa kienyeji.
  • Alikuwa mpiganaji katika vita.
  • Mtu mwenye upendo.
  • Ni mtu mwenye busara.
  • Ni mshauri mkuu wa mtemi Masasa.
  • Mpenda mabadiliko.
  • Ana huruma.
  • Ni mfanyakazi shupavu.
  • Ni mzalendo.
  • Ndiye aliyewapokea Sekai na Takadini.
  • Anafaa kuigwa na jamii
E:Mtemi Masasa
  • Ni mzee wa makamo.
  • Ni mtemi wa kijiji cha watu wa Masasa.
  • Ni mpole.
  • Ni mcheshi.
  • Ni mzee mwenye hekima
  • Ana wake wengi.
  • Ni mpiganaji wa vita.
  • Ni mfugaji.
  • Anafaa kuigwa jamii
F:Shingai
  • Anafaa kuigwa na jamii.
  • Ni jasiri.
  • Ni msichana mwenye msimamo.
  • Ni jasiri.
  • Ni mwanamapinduzi.
  • Ni mke wa Takadini.
  • Ni binti wa mzee Nheriswa.
    G: Tendai
  • Ni mpole.
  • Ni mwanamapinduzi.
  • Ana upendo.
  • Ni mkarimu.
  • Ni mke mdogo wa mtemi Masasa.
  • H:Darai
  • Ni mke wa tatu wa Makwati.
  • Ni mtu makali.
  • Ni mpenda majungu.
  • Ana wivu.
  • Mbinafsi.
  • Ni mama wa Chipo
  • Ana mawazo potofu
  • Ni mnafiki.
  • Hafai kuigwa na jamii.
  • I:Rumbidzai
  • Ni mke wan ne na mdogo kabisa wa Makwati.
  • Ni mtu mkali.
  • Ni mpenda majungu.
  • Ana wivu.
  • Mbinafsi.
  • Ana mawazo potofu.
  • Hafai kugwa na jamii
J:Manyamombe, Mukaru, Chimbiri, Makaure
  • Hawa ni wazee kwa umri.
  • Ni wazee wa baraza la mtemi Masasa.
  • Ni wasimamizi wa mila na desturi za kabila lao.
  • Ni wapiganaji wa vita.
Wahusika wengine:
– Nhamo
– Maishingai
– Pindai
– Ambuya Tungai
– Ambupa Shungu
– Pedeisai
– Mtemi Zvedi
– Tupfumaneyi
– Chengatai
– Chido
– Ambuya Rekai
– Mtemi Chinjeyari
Mandhari
Riwaya hii ya Takadini imetumia ya vijijini katika nchi ya Zimbabwe katika karne ya 19. Katika masimulizi haya ya riwaya mandhari yake inaweza kugusa vijiji vya nchi nyingi za Kiafrika ambazo zipo katika dunia ya tatu. (Nchi zilizoendelea)
Jina la Kitabu
Jina la kitabu ni Takadini. Ni jina ambalo linatoka na jina la mhusika mkuu anayeitwa Takadini. Jina hili pia alipewa na mama yake aliyeitwa Sekai. Jina la Takadini lina maana ya “Sisi tumefanya nini”’?
Jina la kitabu linasanifu yaliyomo katika kitabu hiki kwani kwa kiasi Fulani jina hili linajumuisha mambo yaliyotokea wakati wa uzazi wa mtoto Takadini na matatizo yote waliyokumbana nayo yanayotokana na mila na desturi zinazowabagua watoto na wazazi wa watoto ambao ni Zeruzeru. Takadini yaani “Sisi tumefanya nini?” Linaakisi vilio vya walemavu wote ambao wanatengwa na kuuawa kwa Baraka za wazee wanaosimamia mila hizo. Hawakupenda kuzaliwa viwete, zeruzeru, vipofu na viziwi. Wazazi wao pia hawakupenda iwe hivyo. Kama ndivyo kwa nini kuna adhabu kama hizo? Kwani wamefanya nini? Muumbaji na Mungu na Mungu hana makosa katika uumbaji wake.
Kwa ujumla jinala kitabu linasadifu yaliyomo ndani ya kitabu kwa kuangalia maisha ya mhusika mkuu na matatizo anayopata yanamfanya mhanga yeyote wa mila mbaya aulize swali hili muhimu la SISI TUMEFANYA NINI? Na maana ya swali hili ndilo linatupatia jina la TAKADINI.
KUFAULU NA KUTOFAULU
Kufaulu Kimaudhui
Mwandishi amefaulu kwa kuweza kuonesha matatizo wanayopata watu wenye ulemavu. Mwandishi pia ameweza kuainisha tatizo kubwa linalichangia walemavu kutokubalika ndani ya jamii kuwa ni mila na desturi ambazo zinapandikiza dhana potofu kuhusu walemavu.
Mwandishi pia hakuishia kubainisha matatizo tu, pia ametoa masuluhisho ya matatizo hayo kuwa ni elimu, ujasiri, kuachana na mila na desturi zilizopitwa na wakati.
Kufaulu Kifani
Mwandishi wa riwaya hii amefaulu sana kuonesha ufundi wake katika kusuka kazi yake. Ametumia lugha rahisi ya kueleweka lakini yenye tamathali za semi za kutosha na kuna matumizi ya mbinu nyingine za kisanaa. Vilevile ameweza kuhusu visa na matukio kwa muundo wa moja kwa moja ili kuwapatia wasomaji urahisi wa kufuatilia kwa umakini matukio yote.
Mwandishi pia ameonesha kupevuka sana katika kipengele kizima cha mtindo. Ameweza kutumia nafasi zote, matumizi ya tanzu nyingine kama vile nyimbo na hadidhi ndani ya riwaya.
Amefaulu pia kuteua jina la kitabu ambalo linabeba jina la mhusika na maudhui yaliyomo ndani ya kitabu.
Kutofaulu
Kimaudhui mwandishi ameshindwa kuhusisha walemavu wengine katika kilio cha Takadini yaani tumefanya nini? Mwandishi ameonesha Zeruzeru tu. Angeweza kuonesha matatizo ya mila na desturi yanavyoathiri walemavu wengine.
Kifani mwandishi ametumia idadi ya wahusika bila sababu ya msingi. Idadi kubwa ya wahusika inatakiwa kuwa kielelezo cha upana wa maudhui yaliyomo ndani ya kitabu. Mwandishi pia ameshindwa kuonesha wanakijiji na watu wa kijiji cha asili cha Sekai walipokeaje hali ya takadini kwa kuoa mtu ambaye si mlemavu na kuweza kuzaa mtoto ambaye hakuwa na ulemavu ili liwe funzo kwa jamii zote.
UHAKIKI WA TAMTHILIYA
Jina la kitabu – Ngoswe- Penzi kitovu cha Uzembe
Mwandishi – E. SEMZABA
Mchapishaji – Nyambari Nyangwine Publishers, 2006

Utangulizi
Wasanii kama sehemu ya jamii wanapaswa kushirikiana kikamilifu katika mipango
ya kitaifa. Mipango mingi inahusishwa na mipango mingine ya kisiasa, kiuchumi, na kiutamaduni. Ili mipango hii iweze kukamilika, suala la kujua idadi ya watu ni la msingi.
Ngoswe ni tamthiliya inayoangalia kwa makini suala la uhesabuji wa watu na utayari wa watu wenyewe kuhesabiwa. Aidha tamthiliya inaonyesha hali na wajibu wa watu wanaokabidhiwa dhamana ya kupanga kazi ya kuhesabu watu.
Maudhui
Ngoswe – Penzi Kitovu cha Uzembe ina dhamira mbalimbali zinazojitokeza:
Suala la mapenzi
Tamthiliya ya Ngoswe – Penzi Kitovu cha Uzembe inaliweka suala la mapenzi kuwa “kitovu” kikubwa cha uzembe. Katika kufafanua na kuthibitisha hoja au dhamira hii mwandishi anawatumia Ngoswe na Mazoea. Ngoswe kama kijana wa kiume na ofisa mhesabuji wa watu, anaonekana kuwa na uchu wa mapenzi mara anapomwona Mazoea (uk 5).
Kitendo cha “kupenda” si kibaya kwani ni sehemu ya maisha ya binadamu lakini jambo la msingi kuelewa hapa ni “jinsi na namna ya kupenda”Tatizo kubwa linalojitokeza katika tamthiliya hii kile kinachomfanya afisa Ngoswe kupenda kiasi cha kuharibu kazi. Ngoswe hawezi kulaumiwa kwa kumpenda Mazoea, ila analaumiwa kupenda bila kujizuia na kufika hatua ya kumtorosha Mazoea (uk 24-28). Katika mapenzi yanayoonyeshwa na Ngoswe. Athari zifuatazo zinajitokeza: Ngoswe anapotoroka baada ya kumuiba Mazoea anasahau karatasi za takwimu ya hesabu ya watu kwa vile kitendo cha kumtorosha Mazoea kinamuudhi baba yake, baba huyo anaamua kuchoma moto karatasi za takwimu (uk 28)
Mapenzi ya ngoswe yanaonyesha kuwa ni ya kitoto, na kwavile ni ya kitoto, inaonekana wazi hayakufuata taratibu za mila na desturi zinazofuatwa na wanajamii.
Kutokana na hali hiyo, kazi ya kuhesabu watu inaharibika. Labda jambo la kusisitiza ni kuwa mapenzi ni kipengele tu kilichosaidia kuleta au kuharibu kazi.
Hasara za ulevi
Ngoswe – Penzi Kitovu cha Uzembe inaonyesha tatizo la ulevi linavyochanganya akila na kuharibu kazi nay a kuwa pombe inaathiri mambo mengi.
Ulevi unachelewesha kazi, Mfano wa wazi ni wakati wanapopanga kuanza kazi ya kuhesabu watu, kila wakiwafuata baadhi ya watu hukuta wamekwenda kwenye pombe. Mito mingi anasema (uk 6).
Mitomingi: Haya ni matatizo. Yote hii shauri ya pombe. Sina shaka yuko kilabuni.
Ngoswe: Haitasaidia. Mkewe tu hana habari ya kuhesabu watu, sembuse hao wengine! Kwa leo haiwezekaniki.

Pili Ngoswe na balozi Mitimingi walikunywa pombe aina ya mnazi mpaka wakalewa na kusababisha kuchoma baadhi ya karatasi za takwimu (uk 18-19) ulevi ni jambo la hatari katika kazi na ni lazima upigwe vita.
Umuhimu wa elimu
Elimu ni chombo muhimu kwa jamii kama inatumiwa inavyostahili. Katika tamthiliya hii, suala la elimu linaonekana kutotiliwa maanani sana na wanakijiji ambako Ngoswe alikwenda kuwahesabu. Familia nyingi zanaeleza kuwa watoto hawasomi kwa sababu shule ziko mbali na pale wanapoishi wao (uk16).
Kutokana na shule kuwa mbali yaelekea maendeleo ya kijiji yamebaki kuwa duni. Mfano unaoonekana ni ule wa huduma muhimu kama vile Hospitali kuwa mbali na pale wanapoishi (uk 16)
Ili kupata maendeleo suala la elimu lazima litiliwe mkazo, watu wengi wakielimika wataweza kutumia huduma vyema- kama vile kwenda hospitalini kwa matibabu kuliko kushiriki mitishamba tu.
Lakini kwa upande mwingine elimu imeonyesha kwenye tamthiliya hii kuwa ikitumiwa vibaya haiwezi kuleta faida. Kwa mfano Ngoswe aliyekuwa amepata elimu ya kutosha ameshindwa kuitumia vyema katika kuleta ufanisi wa kazi na kuleta amani na utulivu miongoni mwa wanajamii.g
Ili elimu iweze kuwa ya manufaa ni lazima itumike katika kuibadilisha jamii na kuisukuma mbele katika maendeleo. Na ili kupata maendeleo, lazima shule au huduma nyingine muhimu kama hospitali zisogezwe karibu na watu. Kijiji cha Mitomingi kinahitaji msukumo mkali ili kufikia maendeleo bora.
Malezi na ndoa za mitara
Kijiji kinachojadiliwa katika tamthilia hii kinaelekea kuwa katika mila na desturi za kuoa wake zaidi ya mmoja. Balozi Mitomingi ameoa wake wawili na kuna wanaume wengine waliofanya hivyo.
Suala la kuoa mitara limeonyesha athari mbovu katika malezi na utulivu wa familia nzima. Mwanaume akioa wanawake wengi familia inaongezeka na kuwa kubwa kiasi cha yeye kushindwa wakati mwingine kutoa huduma zinazotakiwa.
Familia ya Mitomingi ina watoto ambao huduma zao zinatia mashaka ndio maana pengine Mazoea aliweza kumkubalia Ngoswe ili kukimbia matatizo yanayojitokeza katika familia yao.
Pia wanawake walioolewa katika mitara hawaelekei kuwa na upendo wa kweli katika jamii yao. Kwa mfano, mama Inda na mama Mazoea hawakuwa wanapendana kwa dhati kwa wake zake wote wawili kwa kina kilekile. Kwa sababu ya kutopendana miongoni mwao ugonvi hauepukiki.
Ikiwa tabia ya kuoa wake wengi ni mila, basi hii ni mila isiyofaa. Sawa na hili pia, mila mbovu ambazo hazifai, kama vile kuchaguliwa mchumba kama ambavyo Mazoea alifanyiwa, sijambogg zuri. Tamthiliya ya Ngoswe inatoa tahadhari na hatari ya kuwa na mitara.
Hatari ya uvivu
Kijiji cha balozi Mitomingi kwa ujumla kinaelekea kuwa na watu wengi wavivu. Suala hili lauvivu linaelekea kuathiri kazi zozote zinazowahusu watu hao. Kutokana na uvivu, jamii ya Mitomingi haina maendeleo. Hakuna shule wala hospitali. Maisha yao ni ya ulevi tu. Watu wanajihusisha zaidi na ulevi kuliko kufanya kazi. (Hapa mwandishi anaitahadharisha jamii kuwa, uvivu ni sumu ya maendeleo).
Imani za uchawi na ushirikina
Jamii ya Balozi Mitomingi inaelekea pia kuwa na imani ya uchawi na ushirikina.

Kwa mfano, wakati wa kuhesabu watu baadhi wanaamini kuwa wachawi ndiyo wanaohesabu watu ili wawaue. (uk, 14),
Mama : “Sasa baba utatuhesabu vipi?”
Mitomingi: “Kwanini?”
Mama : Kama utatuhesabu wewe basi u mchawi”
Mitomingi: “Mbona sikuelewi!”
Mama : “Mchawi ndiye anayehesabu watoto wa wenzie ili awaroge sasa wewe umchawi? Hata kama hu mchawi siwezi kukubali utuhesabu maana siwezi kujua kama nia yako ni mbaya au nzuri.”
Kutokana na jamii ya Mitomingi kuwa na imani hii, zoezi zima la kuhesabu watu linakwama. Hali kadhalika katika jamii hii waliarnini kuwa mtu akifa basi amerogwa. Kama asemavyo mama wa kwanza. (uk. 16) “Wamemroga bure mume wangu. Alikufa akiwa na nguvu zake”.
Kwa ujumla haya ni mawazo ambayo hayana umuhimu wowote kwa jamii zetu. Kufa kwa mtu si kurogwa tu, ni pamoja na kutompeleka hospitalini. Hivyo msanii anatahadharisha jamii kuwa imani hizi potofu lazima zipigwe vita.
Nafasi ya mwanamke katika jamii
Tamthiliya ya Ngoswe imemchora mwanamke katika vipengele mbalimbali. Kwanza, kama chombo cha starehe. Katika kijiji hiki wanaume wanaonekana kuwatumia wanawake katika starehe. Hii inathibitishwa na tabia ya kuoa mitara kila mara ili wanawake watumike kukidhi haja ya wanaume.
Pili, amechorwa kama mzazi, Hapa wanawake wanaonekana wakijishughulisha na kazi za malezi baada ya kuzaa.
Tatu, Amechorwa kama kiumbe. duni. Hapa mwanamke anadharauliwa na mwanaume na akili zake kufananishwa na za mtoto. Mwanamke hathaminiwi na hafikiriwi kuwa anaweza kuchangia jambo lolote la maana. Wakati Mazoea
anatoroshwa na Ngoswe, Mitomingi anauliza (uk. 26),
Mitomingi: ‘ ‘Hivyo na nyie hamkuona dalili zozote juu ya watu hawa wawili?”
Mama Mazoea : “Zilikuwepo “
Mitomingi : Kumbe mliziona mkanyamaza tu!”
Mamainda : “Sasa baba Mazoea tungefanya nini?”
Mitomingi: : “Mngefanya nini? Nyie wanawake akili zenu wote sawa.” Si Mazoea, si mamayake….”
Kauli hii inaonyesha kuwa Mitomingi humthamini mke wake kwa sababu anaona kwamba hana akili za kikubwa. ni kama mtoto wake Mazoea, Tabia hii ya Mitomingi na ya wanaume wengi kuwadharau wanawake ni jambo ambalo lazima lipigwe vita.
Mvutano baina ya mji na vijiji
Mwandishi ameonyesha tofauti za kiutamaduni kati ya maisha ya mjini na yale ya vijijini. Tamthiliya hii inaonyesha athari za maisha ya mjini juu ya yale ya kijijini. Kwa mfano, utulivu wa kawaida wa kijijini tumeona jinsi unavyoingiliwa na fujo za mjini za akina Ngoswe.
Kitendo cha Ngoswe kumtorosha Mazoea bila ridhaa ya wazazi wake ni kinyume na taratibu za vijijini lakini ni jambo la kawaida kwa upande wa mjini na ni kutokana na kitendo hicho, Mitomingi anachoma karatasi za hesabu ya watu. Katika kutatua mvutano huo kati ya miji na vijiji Ngoswe anapendekeza kuwa,
“Hesabu ijayo ifikapo
Sharti vijiji kurekebishwa
Ujinga. Magonjwa na
Umaskini kupigwa vita
Na njia ni moja tu
Kuishi pamoja; kijamaa,” (uk. 29).
Wakati Ngoswe anapendekeza watu kuishi pamoja kijamaa kwa upande wa Mitomingi anaona kuwa kuna umuhimu vilevile kwa watu wa mjini kufundishwa kuishi kijamaa ili waweze kuyajua vizuri maisha ya watu wa kijijini na bila hivyo basi mvutano utaendelea kuwepo. Mitomingi anasema hivi,
“Mijini pia budi wafundishwe kuishi kijamaa maisha yetu kuyajua ama sivyo patatokea matata wawili hawa wakutanapo.” (uk. 30)
Kwa ujumla mwandishi anaona kuwa ili kuondoa mvutano huu kati ya miji na vijiji, ni lazima watu wa mjini wajifunze taratibu za maisha ya watu wa vijijini ambao bado hawajaathiriwa sana na utamaduni wa kigeni
Ujumbe
– Si jambo zuri kuchanganya suala la kazi na starehe au mapenzi; wakati wa kazi uwe wa kazi na wakati wa starehe uwe wa starehe, na starehe ziwe mbali naofisi.
– Wavulana wanaovuruga wasichana siku moja watakamatwa; na wasichana wenyewe wanapewa tahadhari kuwa wasifanye maamuzi bila kufikiri
– Elimu ni kitu cha muhimu sana katika jamii na jamii isipokuwa na watu walioelimika haiwezi kuendelea.
– Ili tuendelee tunahitaji kutupilia mbali ulevi na uvivu katika jamii zetu.
Migogoro
  1. Mgogoro kati ya Ngoswe na wazazi wa Mazoea, unatokana na uamuzi waNgoswe kumpenda Mazoea na kujaribu kumtorosha.
  2. Mgogoro kati ya Mazoea na wazazi wake unatokana na kitendo cha Mazoea kujaribu kutoroka na Ngoswe wakati anajua kuwa alikuwa anataka kuolewa.
  3. Mgogoro kati ya Ngoswe na serikali unatokana na kitendo cha Ngoswe kuharibu kazi ya hesabu ya watu,
Falsafa
Mwandishi anaamini kuwa jamii inaweza kuingia katika matatizo pale mapochanganya vitu viwili kwa wakati mmoja. Hivyo si vizuri Migogoro
kuwatumikia mabwana wawili kwa wakati mmoja.
Msimamo
Mwandishi ana msimamo wa kimapinduzi, kwani amezungumza wazi juu ya matatizo mbalimbali yanayoikabili jamii kama vile umaskini, uvivu, ulevi. tatizo la ndoa za mitara na imani za uchawi na ushirikina.
Fani
Muundo
Muundo wa moja kwa moja umetumika. Tamthiliya imegawanywa katika maonyesho matano na kila onyesho lina kichwa cha kitaswira kinachoendana na yale yanayojadiliwa katika onyesho hilo.
Mtindo
Mwandishi ametumia mbinu ya dayolojia ambapo watu huzungumza wakijibizana na kutenda mambo mbalimbali, Katika kutajirisha mtindo wake, ametumia lugha ya kishairi pia (uk, 29 – 30).
Lugha
Tamthiliya ya Ngpswe Pen^i Kitow cha U^embe imetumia lugha laini (rahisi) na nyepesi inayoeleweka kirahisi. Licha ya hiyo ametumia tamathaU za semi na mbinu zingine za kisanaa. Pia kuna ujenzi wa taswira.
Misemo
– Hebu keti tutupe mawe pangoni (uk. 11).
– Kupeleka chakula ndio unafanya makao kabisa (uk. 1 1) .
Methali
Penye nia pana njia (uk. 22).
TamathaU za Semi
Tashibiha
– Vumbi jekundu kama ugoro wa subiana (uk. 1).
– Hebu kwanza tazama sarawili yake miguuni kama kengele ya bomani, (uk. 7).
– Nilitoka hapa na kujitupa kitandani kama gogo. (uk. 18).
Tasfida
Wala hajarudi kama ingekuwa ni kujisaidia si angekuwa amekwishamaliza? (uk. 21).
Mbinu nyingine za kisanaa
mdokezo
– Mazoea: Sijui … Siwezi… Narnuogopa baba (uk. 22),
– Mltomingi: Usizidl kuniambia mama; Tambitambi mambo yake hakuna
asiyeyafahamu … sasa mama …. (uk. 14).
Ngoswe: “Huyo mtoto wenu wa kwanza anaishi hapa au ….” (uk., 16).
Tunakaii Sauti
Mfano. Ngoswe anacheka. ha! ha!, n.k.
Takriri
– Karibu. karibu (uk. 2).
– Hodi! hodi! (uk. 5).
Taswira
Taswira mbalimbali zimetumiwa na mwandishi katika tamthiliya hii. Msanii ametumia taswira ya mto kwa kuhusisha na matukio ya wahusika. Mwandishi analinganisha mwanzo wa mchezo na kijito. kijito ni mto mdogo sana. Hivyo maelezo ya sehemu hii yanategemea kuwa madogo. Si makubwa. Matatizo yanayoelezwa katika sehemu hii ya awali tu.
Sehemu inayofuata inahusu vijito. Taswira ya vijito inaonyesha kuwa masuala yanayoshughulikiwa kujadiliwa hapa yanaongezeka ingawa bado si mazito.
Sehemu ya mto inaonyesha ukubwa wa shughuli ya Ngoswe. Ngoswe yuko kazini yuko mtoni tayari, yuko katika juhudi ya “kuvuka” kilichoko humo, bila shaka maji ya mto ni mengi (matatizo) na hivyo yeyote atakayeingia mtoni yampasa awe mwangalifu.
Sehemu ya jito inaashiria kuna hatari mno (matatizo). Kuna mengi katika jito. Kulivuka si kazi rahisi. Hatimaye tunaonyeshwa kuwa Ngoswe amezama baharini na amepotea. Tukihusisha na yale yaliyotokea na taswira ya bahari tunasema kuwa Ngoswe amezama, makaratasi ya takwimu yamechomwa moto na Mitomingi kutokana na kosa la kumtorosha Mazoea.
Wahusika
Ngoswe
Huyu ndiye mhusika mkuu katika tamthiliya hii. Ni msomi anayepewa kazi ya kuhesabu watu. Lakini kutokana na tamaa ya mwili wake anaharibu kazi baada ya takwimu zote kucttgmwa” moto na Mitomingi. Kutokana na kitendo chake cha kujaribu kumtorosha ‘Mazoea bila ridhaa ya wazazi wake. Ngoswe ni mfano wa watu wanaochangartya kazi na starehe. Matokeo yake ni kuharibu kazi. Hivyo hafai
Kuigwa.
Ngengemkeni Mitomingi
Huyu ni balozi na baba yake Mazoea. Ni mzee ambaye ameshikilia ukale na anayependa ndoa za mitara. Huyu anachoma karatasi za takwimu kutokana na Ngoswe kujaribu kumtorosha mtoto wake Mazoea.
Mazoea
Msichana mwenye umri kati ya miaka 18-20 ambaye ni mtoto wa balozi Mitomingi. Mazoea anawakilisha wanawake wasio na misimamo maalum katika mapenzi.
Mama Inda na Mama Mazoea
Hawa ni wake wa Mitomingi na walezi wa Mazoea.
Mandhari
Mandhari ya kijijini imetumika. Kijiji hicho kipo katika nchi ya Tanzania. (Aidha inawezakana kikawa kijiji chochote katika nchi zinazoendelea).
Jina la Kitabu
Jina la kitabu Ngoswe Penzi Kitovu cha uzembe linasadifu vizuri yale yaliyomo ndani ya kitabu hiki. Ngoswe ni jina la mhusika mkuu ambaye msanii anaonyesha jinsi kuendekeza kwake penzi kulivyomharibia kazi yake ya kuhesabu watu.
Kufaulu kwa Mwandishi
Mwandishi ameonyesha kwa Masi kikubwa kuyajadili matatizo yanayozikumba jamii zetu katika fani mbalimbali za maisha. Matatizo hayo ni kama uchawi. uzembe, n.k. Pia ametumia lugha rahisi inayoeleweka.

Jina la kitabu: – Kilio Chetu
Waandishi – Medical Aid Foundation
Wachapishaji: TPH
Mwaka: 1996
Utangulizi:
Kilio Chetu ni tamthiliya iliyotungwa na Medical Aid Foundation. Katika tamihiliya hii kama asemavyo Vivian Mmari, Makamu Mwenyekiti wa Medical Aid Foundation katika utangulizi wake, Inajaribu kjvunja ukimya uliotawala miongoni mwa wanajamii katika kutatua matalizo makubwa ya kijamii yatokanayo na mahusiano ya kijinsia.
Tunasikia sauti ya jitimai itolewayo na watoto. Sauti iliyojaa sononeko na shutuma dhidi ya wazazi, walezi na watawaJa wenye kuufumbia macho msiba huu mkubwa wenye kuwaangamia.
Tunasikia sauti za vilio vya watoto wanaodai haki ya kuelimishwa kuhusiana na mambo yanayoweza kuathiri maisha yao. Wanataka wazazi, walezi na watawala wao kuwa wazi ill kunusuru maisha yao.
Hii ni tamthiliya inayopendekeza na kuibua mjadala miongoni mwa wanajamii kuhusiana na suala hili muhimu. Ni maoni ya mwandishi kwamba wakati tulionao sasa sio sawa na ule wa zamani. Mambo mengi yamebadilika, hivyo hata medani za vita hazina budi zibadilike katika kutatua matatizo ya wakati huu. Ushauri unaotolewa katika tamthiliya hii ni kwamba zile kuta zinazozuia mawasiliano ya wazi baina ya wazazi, walezi na watoto wao lazima ziangushwe.
Ni imani ya mwandishi wa tamthiliya hii kwamba, matatizo kama yale ya mimba katika umri mdogo, magonjwa ya zinaa kama UKIMWI, na kusambaratika kwa maadili katika jamii yanaweza kutatuliwa kwa kuwapa watoto elimu ya jinsia badala ya kuwajengea hofu na vitisho ambavyo kusema kweli vimedhihirika kuwa ni silaha duni katika mapambano haya.
Maudhui
TamthiJiya ya Kilio Chetu inabeba maudhui yanayozungukia mambo kadha wa kadha yahusuyo gonjwa hatari la UKIMWI, Kwa kutumia mbinu mbali mbali, mwandishi amelijadili kwa kina suala la malezi kwa ijana/watoto. Anakemea vilivyo suala zima la mahusiano ya kijinsia wakati huu wa hatari tulionao. Pengine ni vizuri tukazipitia dhamira zilizojitokeza katika tamthiliya hii moja baada ya nyingine.
Dhamira
Dhamira kadhaa zimejitokeza katika tamthiliya hii na zinajionyesha wazi kupitia migogoro anayoijenga mwandishi na pia matendo ya wahusika.
Dhamira kuu
Elimu ya jinsia
Umuhimu wa elimu katika familia, hususani elimu ya jinsia ni suala ambalo limetawala katika tamthiliya hii. Kwa upande mmoja kuna wazazi/walezi ambao wapo teyari na wameamua kuvunja ukimya uliokuwepo kati yao na watoto wao na kuzungumza nao waziwazi juu ya masuala ya mahusiano ya kijinsia na hadhari zake. Wahusika hao ni mjomba na baba Anna. Mathalani baba Anna anasema:-
Hili ndilo nimefaulu mwenzenu Nimemwambia mama Anna akae na mabinti nami nikae na wakiume …… Tumewaelimisha juu ya madhara ya tabia hiyo…”(uk. 10).
Kwa upande mwingine kuna wazazi/walezi wanaoshikilia ukale. Hawa bado wanaamini kwamba kutozungumza na watoto habari zinazohusu ngono kutawazuia wasijihusishe na mambo ya kujamiiana mapema. Mama Suzi na baba Joti ni watetezi wa msimamo huu. Matokeo ya msimamo huu ni kupoteza watoto. Kwa mfano, mama Suzi anasema:- “Tena ishia hapo hapo kaka! Huko si ndiko kunifundishia mwwanangu habari za ngono, ilitoka wapi hiyo?..”(uk.9).
Matokeo ya msimamo hii miwili imejadilliwa barabara katika tamthiliya hii. Mjadala unaohitimishwa kwamba ni bora watoto wakaelimishwa na kupewa habari sahihi kuhusiana na ngono na afya zao za uzazi kuliko kuwatia hofu na kuwatisha kwani hiyo kamwe haisaidii.
Mwandishi kwa kumtumia kumtumia Anna, binti ambaye wazazi wake wameamua kuvunja ukimya na kuongea naye waziwazi juu ya mambo ya mapenzi na hatari yake anatanabaisha faida za elimu hii. Anna mara zote anachukua uamuzi wa busara huku akijiamini kwa kila analolisema. Hii ni kutokana na msingi imara aliopewa na wazazi wake baada ya kuamua kuwa wazi kwake. Kuonensha namna Anna anavyopikwa akaiva kufuatia elimu ya jinsia aliyopewa na wazazi wake, mwandishi anamchora akisema:-
Hujui, mjinga mkubwa we! Hujui kama kuna madhara mengine. Hujui magonjwa ya zinaa wewe, hujui kisonono, kaswende, na mengine kedekede, Haya hata juu ya UKIMWI hujui? Hebu nitolee uchafu wako mie ptuu!”(uk.25).
Kauli hii ya Anna inaonyesha jinsi ambavyo watoto, wawe wa kike au wa kiume, wakielimisha na wazazi, kwa vile ndio walimu wao wa kwanza, wanaweza kujijengea uwezo wa kujiamini na hivyo kuepukana na vishawishi vinavyoweza kusababisha maambukizo ya UKIMWI. Wanapotishwa bila kuambiwa ukweli wa mambo kwa visingizio vya makatazo ya dini, mila na desturi wanakuwa mbumbumbu katika suala zima la kujamiianana madhara yake ni kama tuonavyo kwa wahusika Joti na Suzi katika tamthiliya hii.
Dhamira ndogondogo
Zipo dhamira nyingine kadhaa ambazo zimejadiliwa chini ya dhamira kuu, nazo ni:-
Mapenzi katika umri mdogo
Kimsingi watoto wadogo (vijana wadogo) bawapaswi kujihusisha na mambo ya ngono mpaka hapo umri wao unapowaruhusu kuoa au kuolewa. Huu ndiyo msingi na msimamo wa mila na desturi za kiafrika na hata dini. Kinyume chake watoto wanaanza kushiriki vitendo vya kujamiiana katika umri mdogo jambo ambalo ni hatari kwa maisha yao. Hiyo ndiyo hali halisi. Ni mara ngapi unasikia wanafunzi wa shule wanafukuzwa kwa sababu ya kubeba mimba? Hali hii imesawiriwa barabara katika tamthiliya hii ya Kilio Chetu. Watoto wa shule ya msingi kama vile Joti, Suzi na wengine wanaonekana kushiriki vitendo vya kujamiiana katika umri mdogo (uk. 16 -17, 19 – 21), Baya zaidi baadhi ya watoto wanashiriki matendo ya kujamiiana na wanawake au wanaume wanaowazidi umri., na pengine wenye wapenzi wengine jambo ambalo ni hatari kwa maisha yao. Kwa mfano, katika tamthiliya hii, mwandishi anatanabaisha kuwa Joti alikuwa anaparamia mpaka wasichana wakubwa wa mitaaani. Kwa maneno yake mwandishi anasema:-
“Sasa ndiyo kuparamia mpaka wasichana wakubwa wa mtaani? Fikiri juu ya Chausiku, yule msichana mjuvi wa mji, ambaye pia anachukuliwa na yule Mpemba muu^a duka” (uk. 23).
Suala hili linaweza kuwa limechochewa pamoja na mambo mengine, kuzagaa kwa sinema za utupu, vijalida vanavyohamasisha ngono na zaidi ya yote, kuna mtandao wa internet ambao watoto wadogo wanatumia kuangalia picha za utupu zinazowahamasisha kufanya ngono. Mwandishi ameisawiri hali hii barabara. Anawaonesha vijana wanne, Joti, Jumbe, Choggo na Mwarami wakikumbushana kwenda kuangalia picha za -X, ingawa kuna zuio kwamba picha hizo ni kwa wakubwa tu (uk. 17-18).
Mapenzi na ndoa
Pamoja na kuwepo janga la UKIMWI bado watu wameendelea kutokuwa waaminifu katika ndoa zao. Wanandoa wanathubutu kutembea nje ya ndoa bila woga. Mwandishi anasawiri hali hii kwa kumtumia mama Joti. Mama Joti analalamika kuwa ndoa yake imeingiliwa. Hivyo kama suluhisho anaamua kununua kanga zenye maandishi yanayomsuta huyo anayeingilia ndoa yake. Mfano maneno
“Makapera kibao mume wangu wa nini” (uk. 7).
Swali la kujiuliza hapa ni je hili litasaidia? UKIMWI je? Mwandishi pia anafichua fikra za walio wengi kwamba wanaougua UKIMWI ni makapera na sio wanandoa (uk. 7). Hata hivyo dhana hii sio sahihi maana UKIMWI hauchagui wenye ndoa au wasio na ndoa.
Huduma kwa wenye Ukimwi
Mwandishi anajadili suala hili. Anatueleza kwamba.kugusana kwa kawaida na mgonjwa kugusa nguo zake na kupeana mikono na mgonjwa hakuambukizi mtu ugonjwa huo. Aidha anajadili umuhimk wa kumtunza mgonjwa wa UKIMWI. Ingawa hataji waziwazi, lakini anaongelea suala hili kwa kumtumia mhusika Mjomba (uk. 34). Mjomba anawashauri baba na mama Joti kumpa matunzo mazuri na upendo mgonjwa Joti. Anashauri mgonjwa asitengwe maana ugonjwa huu hauambukizwi kwa njia ya kuvuta hewa ya mgonjwa au kula naye. Zaidi mwandishi anasema;
mgonjwa apewe chakula bora na yanapojitokeza magonjwa mengine kama malaria, apelekwe hospitali kwa tiba ”(uk. 34)
na upendo mgonjwa Joti. Anashauri mgonjwa asitengwe maana ugonjwa huu hauambukizwi kwa njia ya kuvuta hewa ya mgonjwa au kula naye.Zaidi mwandishi anasema;
mgonjwa apewe chakula bora na yanapojitokeza magonjwamengine kama malaria,apelekwe hospitali kwa tiba.”(uk.34).
Tiba ya Ukimwi
Kumekuwepo na mikanganyiko mingi miongoni mwa wagonjwa wa UKIMWI na jamaa wanaowauguza.Wengi wao hawataki kuamini kwamba wanaugua UKIMWI hata baada ya vipimo vya hospitali kuthibitisha hivyo.Badala yake hutawanya rasilimali zingewasaidia wao wakati wanaugua,na pengine familia zao baada ya kifo,katika kutafuta tiba za asili,Mwandishi akimtumia Mjomba analijadili jambo hili na kupinga waziwazi tabia ya kutapatapa anasisitiza tabia ya kuukubali ukweli ingawa unauma.
……………ugonjwa huu hauna tiba.Ushahidi hupo wazi kabisa kwa kadri tunavyowaona wanaopata ugonjwa huu. Kwa hiyo si busara pia kuongeza matatizo hali ukweli tunaujua…”(uk.34).
Dhamira nyingine zilizojitokeza ni : athari zaakiw marafiki, Nafasi ya mwanamke katika jamii, Mila na desturi, n.k.
Nafasi ya mwanamke katika jamii
Waandishi wa tamthiliya hii ya kilio chetu wamemchora mwanamke katika nafasi na sura wa kadha wa kadha. Mathalani, wanamchora mwanamke akiwa mhuni na mwenye dhima ya kukidhi matamanio ya wanaume. Ni kwa kumtumia mhusika chausiku kwa mfano, waandishi wanatuonyesha namna mwanamke anvyotumiwa na mwanaume katika dhima hii. Chausiku licha ya kuwa mpenzi wa mpemba mwenye duka pia ni mpenzi wa Joti, kijana mdogo aliye bado mwanafunzi wa shule ya msingi. Mhusika mwingine mwenye kudhihirisha surah hii ya mwanamke ni suzi. Huyu ameumbwa katika sura ya kukidhi tama za mwili wa Joti.
Kadhalika, mwanamke anaonekana kuwa mnyonge na duni kiasi kwambahana uwezo wa kuchukua hatua zinazostahili anapoona ndoa yake imeingiliwa. Hili ni tatizo kubwa linalomkabili mwanamke hasa kwa wakati kama huu ambapo dunia imekumbwa na balaa la UKIMWI. Tunamuona mhusika Mama Joti angundua tatizo katika ndoa yake lakini honyeshi ujasiri wa kukaa na Baba joti na kulizungumzia suala hili la unyumba wao, nabadala yake anakimbilia kununua khanga ili kumsuta huyo “kidudu mtu” anyeisakama ndoa yake. Nafasi aliyonayo mwanamke katika asasi ya ndoa ndiyo haimruhusu wala kumpa mwanamke ujasiri wa kukaa na kuzungumza na mmewe kuhusu masuala haya.
Kwa upande wa pili wa shilingi, mwanamke katika tamthiliya hii anapewa nafasi kuwa mtu mhimu na wa kutegemewa katika malezi ya familia. Mathalani wahusika wanawake Mama suzi na Mama Joti wanaonekana kutoa mchango mkubwa katika malezi. Wako makini katika kufuatilia mienendo ya vijana wao na kuhakikisha kwamba wanakua katika misingi inayofaa. Tatizo pekee tunalohisi limechangia kwa wao kutofanikiwa katika ama yao ni njia walizotumiakatika malezi. Pengine wangeweza kufaulu kama wangetumia njia ya kuzungumza na kuwaelimisha watoto wao kama walivyofanya Baba na Mama Anna.
Aidha, mwanamke katika tamthiliyaa hji, imejengwa akiwa ni mwenye kuwa na msimamo Thabiti kama amejengewa msingi imara katika malezi yake, mwakilishi wa mwanamke kama kiumbe alien a msimamo madhubuti katika tamthiliya hii ni Anna. Anakataaa kufanya mapenzi katika umri mdogolicha ya kudanganywa kasha kutishwa na mhusika Mwarami. Ingawa ni wachache, lakini wapo wanawake wa aina ya Anna katika jami
Lakini pia, kupitia mhusika Anna, mwanamke anajitokeza kama mshauri na muelimishaji rika. Katika kutimiza Dhima hii, Anna anamshauri mwarami kwamba asikimbilie sut kabla ya kuvaa nepi. Maana yake ni kwamba hana
budi kusubiri hadi hapo wakati utakapofika ndipo aingilie masuala ya mapenzi, na sio kufanya hivyo katika umri mdogo alionao.
Mila na desturi
Suala l mila na desturi zinazofungamana na ukale pia limechukua nafasi katika tamthiliya hii. Moja ya sababu zinazowafanya baadhi ya wahusika katika tamthiliya hii ya kutokubaliana na ushauri wa kuongea na watoto wao mambo yanayohusu kujamiana nipamoja na mila na desturi, Mila hizi, haziruhusu wazazi kuongelea masuala hayo na watoto wao wa kuwazaa.
Hata hivyo kushikilia mila na desturi hizi katika enzi hizi za UKIMWI ni sawa na kusema waache watoto afe kwa UKIMWI. Ni kutokana na athari jamii inazoweza kuzipata, waandishi wakasema pamoja na kwamba mila na desturi zetu haziruhusuwatu wazima, has wazazi, kujadili masuala wanayoyaita ya wakubwa na watoto wao wa kuwazaa, bado tunapaswa kuliangalia suala hili kwa jicho pevu. Pengine tuamue kuachana na mila na desturi hizo kwa lengo la kulinusuru taifa la kesho, Lazima jamii ikubali kuachana na maila ana desuri zilizopitw na wakati na kangalia njia ya kuwanusuruwatoto juu ya maambukizi ya UKIMWI.
Migogoro
Tamthiliya ya kilio chetuimejengwa juu ya migogoro kadhaa. Migogoro mingi ni kati ya kundi linaloshikilia ukale na lile linalotaka mabadiliko katika malezi ya watoto kuhusiana na elimu ya mahusiano ya kijinsia.
Mgogogoro wa kwanza ni kati ya mama suzi na bintiye. Mgogoro huu unatokana na vidonge vya kuzuia mimba kukutwa katika mfuko wa nguo za shule za suzi. (uk.7). mama suzi anchukua hatua ya kumwadhibu suzi kama mwarubaini wa kukomesha tabia hii bila kutmbua kwmba hofu na vitisho haviwezi kufua dafu mble ya silica ya mwili.
Mgogoro huu unaingiliwa na watu watatu. Baba Joti, ambaye anmuunga mkono mama suzi.Ili kusuruhisha mgogoro huu rai inatolewa kwamba lazima akina Mama Suzi wabadilike na wavunje ukimya uliotawala miongoni mwao kama kweli wamedhamilia kutatuamatatizo yanayoweza kuwaangamiza waoto wao.
Mgogoro mwingine ni kati ya Joti na mpenzie (Chausiku). Huu ni mgogoro unaotokana na tabia ya Joti kuwa na wasichana wengi anaotembea nao. Chausiku anamkaripia Joti kwa tabia hiyo chafu na anahahidi kumuunguza Joti na wasichana wake kwa moto hasa baada ya kugundua kwamba vitu anavyomhonga Joti anavitumia kwa wasichana wake wengine (uk. 22). Chausiku anasema:-
me nakununulia fulana ya mazoezi wewe unahonga kinyago chako kile…… Nikikupa hela ya kununua peni we unanunulia bazoka visichana vyako”
Pia kuna mgogoro kati ya Mwaratni na rafikize ( Joti na Jumbe) juu ya suala la ngono, Mwarami na Anna juu ya suala la kufanya ngono katika umri mdogo, Suzi na Anna juu ya suala la utoaji mimba nk.
Ujumbe na Maadili
Baada ya kuisoma tamthiliya hii tunapata rundisho kuwa kweli “Asiyefunzwa na wazazi hufunzwa na Ulimwengu” ikiwa na maana kuwa mafunzo wayapatayo watoto toka kwa walezi wao ni bora na ndiyo yawasaidiayo kuishi kwa kujiamini na kutohadaika na mambo yasiyofaa. Hivyo si vizuri kuwanyima fursa hiyo kwa kisingizio cha dini, mila, desturi au sababu nyingine yoyote.
Mwandishi anatoa ujumbe kwamba ugonjwa wa UKIMWI hauenezwi kwa njia za kugusana au kula na mgonjwa. (uk. 34) bali ni kwa njia ya kujamiiana na mtu mwenye ugonjwa huo. Ujumbe huu unasawiri mazingira yetu kwa sasa ambapo kuna ongezeko kubwa la maambukizo ya ugonjwa wa UKIMWI. Hivyo anatoa wito kwa wazazi na walezi kutofumbia macho hali hii bali wawe wazi kwa watoto wao kwa kuwapa elimu ya kijinsia na jinsi ya kuepuka ugojwa huu. Kwani hauna kinga wala tiba.
Mtazamo na msimamo wa mwandishi
Msanii anautazama ulimwengu kwa jicho pevu na yakinifu. Anauona kama kitu kinachobadilika, hivyo hata jamii inapaswa kubadilika. Anayachunguza mazingira yanayo mzunguka mtoto katika zama hizi na kugundua kwamba watoto wako hatarini kuteketea kutokana na kukosa habari zozote za kuwasaidia. Mwandishi anatoa msimamo ambao ni tofauti na wazazi/walezi wengi. Msimamo wa kuvunja ukimya na kuzungumza na watoto kwa kuwapa elimu ya jinsia ili kuwanusuru wasiangamie.
Falsafa ya Mwandishi
Mwandishi anaamini kwamba kuwapa watoto elimu ya familia ikiwa ni pamoja na elimu ya jinsia si kuwafundisha umalaya kama wanavyoeleza wapinzani wa hoja hii. Badala yake, ni kuwafanya watoto wajitambue na kuyaelewa barabara madhara ya kujiingiza katika matendo ya kujaamiiana katika umri mdogo, Hii ndiyo njia pekee ya kuwanusuru vijana/watoto dhidi ya “dubwana” linalotishia maisha yao. Hii ndiyo falsafa ya mwandishi wa tamthiliya hii.
FANI
Tamthiliya ya Kilio Chetuimedhihirika kuwa ni mojawapo ya tamthiliya zenye utajiri wa vipengele vya kifani. Mwandishi amtumia vipengele kadha wa kadha vya fani.
Katika kufikisha maudhui yake kwa walengwa. Vipengele vya fani ambavyo vimejitokeza mara kwa mara katika kazi hii ni hivi vifuatavyo:
Wahusika
Wahusika wa fasihi ni watu ama viumbe wanaowakilisha tabia halisi za watu katika jamii. Tamthiliya ya Kilio Chetu ina jumla ya wahusika kumi na wawili, na wengi wao karibu wana hadhi sawa kiasi kwamba sii rahisi kuwatenga katika makundi ya wahusika wakuu na wadogo kama tulivyozoea.
Wasifu wa Wahusika
Mama Suzi:
Huyu ni mama yake Suzi. Ni mwenye kushikilia msimamo wa kizamani, kwamba mzazi hawczi kuongea na mwanae masuala ya kujamiiana (uk. 6). Haamini kwamba watoto wadogo, kwa mfano, wanaosoma darasa la tano wanaweza kuwa wameanza tabia ya kujamiiana (uk. 5). Kwa maneno yake anasema:
“Fausta alikuwa mtoto sana. Mtoto wa darasa la tano. Mambo hayo asingeyajua” (uk. 8.)
Mama Suzi anawiakilisha kundi la wazazi ambao hawaamini katika kusema na watoto wao mambo yanayoweza kuhatarisha maisha yao, kwa mfano, anapomkuta mwanae Suzi ana vidonge vya kuzuia mimba anachukua jukumu la kumpiga badala ya kumwelimisha juu ya madhara yake (uk. 7 – 9). Haamini kwamba binti mdogo kama Suzi anaweza kuyafahamu mambo ya kujamiiana mpaka anapomkamata na vidonge vya kuzuia mimba. Ndipo anasema:
“Mwanetu huyu keshakua sasa anabugia vidonge vya kuzuia mimba … wewe unataka kuniumbua mie, we mbwa mweusi… ” (uk. 8).
Suzi
Huyu ni mtoto wa mama Suzi. Ni binti mdogo anayesorna darasa la sita. Ni mpenzi wa Joti, mwanafunzi mwenzake. Amekwisha jiingiza katika masuala ya mapenzi katika umri huu mdogo kinyume na matarajio ya mama yake. Mwanzoni mama yake hakuwa na habari kuhusiana na tabia hii ya Suzi hadi alipomkamata na vidonge vya kuzuia mimba (uk. 8). Anamwogopa mama yake sana lakini hawezi kushinda nafsi yake iliyokwishatekwa na mambo ya ngono kutokana na ukosefu wa elimu juu ya mambo haya. Anapata mimba na inaelekea ana UKIMWI kwani Joti aliyempa mimba hiyo imedhihirika kuwa ana UKIMWI.
Baba Joti
Huyu ni baba yake Joti kijana ambaye amepata ugonjwa wa UKIMWI kutokana na kijiingiza katika mambo ya mapenzi akiwa mwenye umri mdogo. Ni jirani yake na akina Mama Suzi. Kama alivyo Mama Suzi, Baba Joti pia haamini katika kuwaelimisha watoto kuhusiana na masuala ya kujamiiana. Anamwona Suzi kuwa ni “kitoto kidogo” kama alivyo mwanae Joti hivyo kumpa elimu ili aifahamu jinsia yake na ajijue alivyo ni kumharibu.
Sado ameshikilia msimamo wa kizamani kwamba wazazi hawawezi kukalishana kitako na watoto wao na kuwaeleza habari za ngono (uk.10). Kwa mawazo yake,dawa peke ya kuwadhibiti watoto wasijiingize katika masuala hayo ni viboko au mijeledi tu (uk. 10).
Mama Joti
Huyu ni mke wa Baba Joti na mama yake Joti. Anaamini kuwa watoto wanajua makubwa maana “Wembamba wa reli treni inapita” (uk. 6). Hakubaliani na kitendo cha kumkingia kifua mtoto maana si rahisi kujua huko waendako wanafanya nini (uk. 6). Ndoa yake imo matatani kufuatia kuingiliwa na nyumba ndogo yeye anaita “Kidudu mtu” (uk. 7).
Mjomba
Ni kaka yake Mama Suzi. Ana upeo rnpana wa kuelewa mambo. Anafahamu ulimwengu wa sasa ulivyo. Maoni yake ni kwamba watoto wapewe elimu ya familia, ikiwa ni pamoja na elimu ya jinsia ili waweze kujua kinagaubaga juu ya mambo yahusuyo mapenzi na hatma yake. Anamini kwamba hii itasaidia kuwaonesha watoto madhara ya kufanya mapenzi kabla ya ndoa. Ana ushauri mzuri, anamshauri Baba Joti asihangaike kwenda kwa waganga wa jadi kwa ajili ya tiba ya Joti aliyegundulika kuwa ana UKIMWI. Badala yake anashauri Joti apewe matunzo mazuri ili aweze kuishi kwa matumaini (uk. 34).
Baba Anna
Kama mjomba, Baba Anna pia ana upeo mpana wa kuelewa mambo. Yeye na mkewe, mama Anna, wameweza kukaa na watoto wao na kuwaelimisha juu ya madhara ya tabia ya kufanya mapenzi katika umri mdogo. Kwanza kwa watoto wenyewe na pia kwa familia nzima na hasa kwa wazazi wao (uk. 10). Anaamini kwamba iwapo watoto wataelimishwa barabara kamwe hawatathubutu kujihusisha na masuala ya kujamiiana.
Jirani
Ni jirani yake Baba Joti. Hana imani na matokeo ya vipimo vya hospitali hivyo anashauri wampeleke Joti kwa “mafundi” zaidi wa tiba. Huyu anawakilisha wananchi wengi ambao hawataki kuamini kwamba UKIMWI upo katika jamii, na mtu ukimpata sio kwamba amerogwa.
Chauslku
Ni msichana wa mtaani, jirani na akina Suzi. Si msichana mzuri kitabia. Anafanya mapenzi na watoto anaowazidi mbali kwa umri. Ni mjuvi wa mji na anachukuliwa pia na Mpemba mwenye duka.
Chogo, Mwarami na Jumbe
Wavulana wanaosoma pamoja na Joti. Kama Joti, nao wamekwishajiingiza katika mapenzi na wasichana. Wana tabla ya kuangalia magazeti ya picha za uchi na sinema za “X”. Wana tabia ya kukaa vijiweni na mazungurnzo yao ni kuhusu masual,.a ya ngono.
Joti
Mwanafunzi wa shule ya msingi darasa moja na akina Suzi, Chogo Jumbe na Mwarami. Ana mahusiano ya kimapenzi na wasichana kibao, kwa mfano Suzi, Chausiku, Yoranda, Gelda na Sikujua. Kwa sababu wazazi wake hawakuongea naye ili kumpa elimu juu ya athari za ngono aliendelea na tabia hii hadi akaukwaa UKIMWI
Muundo:
Tamthiliya ya kilio chetu imechuka muundo wa moja kwa moja, yaani sago. Visa vinaelezwa kwa mtiririko bila kukatizwa. Mchezo unaanzia katika sehemu ya kwanza ambapo maelezo kuhusu kuingia na dubwana (UKIMWI) katika kisiwa kunaelezwa. Sehemu ya pili intujulisha juu ya kifo cha Fausta na pia habari za Suzi kufanya mapenzi zinajulikana kufuatia kukutwa na vidonge vys kuzuia mimba katika mfuko wake. Ni katika sehemu hii mjomba na baba Anna wanaelezea umhimu wa elimu ya jinsia ili kuwanusuru watoto na janga hili la UKIMWI.
Ni katika sehemu ya tatu na ya nne inpodhihirika kwamba wanaoitwa watoto si watoto tene maana wameshajiingiza katika mambo ya ngono, na hivyo wako hatarini kuangamia. Mahusianao ya kati ya joti na Suzi, na wasichana wengine kama vile Chausiku, Yoranda, Gelda na Sikujua yamefunuliwa katika sehemu hizi. Aidha, kwa kututmia mhusika Anna, inaoneshwa katika sehemu ya nne, namna motto aliyepwa elimu ya jinsia anavyoweza kukabiliana na vishawishsi na hivyo kuepukana na balaa la UKIMWI
Sehemu ya tano, suzi anagundulika kuwa na mimba ya Joti . sehemu ys saba intupeleka nyumbani kwao Joti ambapo inadhihirika kwamba joti anaugua UKIMWI na ushsuri unatolewa na mjomba kwamba apewe matunzo mazuri ili aweze kuishi kwa matumaini.
Mtindo:
Mwandishi wa tamthiliya hii amedhamilia kuifanya tamthiliya yake iwe na umbo la kiafrika kufuatia kutumia baadhi ya vipengle vya sanaa za maonyesho za kiafrika katika tamthiliya hii ya kilio chetu. Baadhi ya vipengele hivyo ni pamoja na matumizi ya nyimbo, (uk.1)……, niendelee, nisiendelee?……au mmechoka? (uk.113). pia katika uk. 36, mwandishi anamalizia …Na hadithi yangu imeishia hapo.
Mwandishi pia amemtumia mtambaji kutoa maelezo na ufafanuzi kuhusu matndo ya wahusika na matukio katika tamhiliya yake , mtindo uliozoeleka.
Aidha, mwandishi ametumia mtindo wa diologia. Amefaulu kuleta diologia inayovutia na kuaminika baina ya wahusika.ni diologia ambayo, kwa kweli, ametumia maneno machache lakini yaliyoteuliwa kwa ufundi na ustadi mkubwa sana.
Matumizi ya lugha:
Mwandishi wa tamthiliya hii ya kilio chetu ameonesha ustadi mkubwa katika uteuzi wa lugha ya kutumia. Ametumia lugha inyowafanya wasomi watafakari kwa.
Makini kile wanachokisoma, Lugha iliyotumika ni nyepesi kwa hadhira lengwa, yaani watuwa kawaida, hasa wazazi la walezi. Aidha ni lugha iliyoshehenezwa tamathali za semi na mbinu nyingine za kisanaa
Methali,
“Asiyefundwa na mamaye hufundwa na walimwengu” (uk.36)
“Wembamba wa reli treni inapita “(uk. 6)
Misemo;
“….kukimbilia suti na nepi hujavaa” (uk.26)
“Mapenzi ni tiba” (uk. 22)
: Nakuwa nyumanyuma Kama koti” (uk.4)
Útakatifu wa usoni” (uk.4)
Nahau
”kufa kwa kunyaga nyaya” (uk.4)
Matumizia ya lugha ya kingereza na asili
Mwandishi ingawa ni Kwa kiasi kdogo, ametumia lugha ya kuchang’nya lugha ya Kiswahili na kingereza. Lengo hasa la kuchanga’nya lugha lilikuwa ni kusawiri namna nijana weing wa siku hizi wananyoongea Kwa kuchanga’nya Kiswahili na kingereza. Mfano mzuri 9uk.16)
“Ndo ume-come sio?”
Kwa upande wake, lugha ya asili haijatumika katika mazungumzo ya kawaida. Imetumika tu katika wimbo wa maombolezo (uk.35)
Tamathali za semi.
“Mbona unakuwa mgumu Kama mpingo”? (uk.5)
“Miti inayoungua Kama mabua” (uk.6)
“…..Wakapukutika Kama majani” (UK 3)
Sitiari
“Ndio wa kumvumilia buyu nguru anayechimba ndoa yangu” (uk.7)
“Huyu kinyago wako anakimbia nini?” (uk. 21)
Mbinu nyingine za kisanaa
Onamatopea
“Wacha moyo unipwite pwi, pwi, pwi,” (uk .16)
“Basi vupu nikadondoka….” (uk. 16).
Takriri;
“Piga domo, piga domo” (uk.16).
“Watu walipukutika, wakapukutika Kama majani ya kiangazi; wakapukutika” (uk
.1).
UJENZI WA TASWIRA
Mwandishi anatujengea taswira ya Dubwana lililoleta balaa kisiwani (uk. 1).
Anaeleza kwamba kila mtu aliyeguswa na dubwana hili alipata madhara. Watu waliotoka mapele, wakaharisha, wakanyonyoka nywele, wakakonda na kupoteza uzito kabla ya kufa. Haya ni maelezo yanayomfanya msomaji ajenge woga juu ya dubwana hili yaani UKIMWI.
Mandhari
Mandhari katika tamthilia ni ile sehemu au mazingira ambamo makutano yanatokea. Mandhari ya tamthilia hii ni ya mjini. Hii inathibitishwa na mhusika jirani anaposema:
Mie toka siku ile niwaone hospitali sijakaa mjini. Nilikwenda zangu shamba kupambana na nyani wala nafaka” (uk.32)
Lakini pia habari za kuangalia sinema za “X” (uk.18) zinatuthibitishia mandhari ya mahali matendo haya yanapotendeka ni ya mjini. Zaidi ya hapo, lugha inayozungumzwa na wahusika vijana kama vile Joti, Jumbe, Chogo na Mwarami ni lugha ambayo imezoeleka mazingira ya mjini kulIko vijijini (Rejea kwa mfano mazungumzo yao (uk.16).
Tunaelezwa pia kwenye tamthilia hii kwamba mhusika Mwarami alikuwa akimnunulia Anna soda na mihogo kule uwanja wa Sabasaba (uk.26). Zaidi Anna anaeleza katika wimbo wake kuwa hataki pesa za wanaomhonga wala lift zao (uk.27). Ni wazi kwamba uwanja wa Sabasaba upo mjini na lift kwa akina dada, hasa wanafunzi zinatolewa mjini kuliko vijijini.
Jina la kitabu
Kilio chetuni jina la kitabu linalo akisi yale yaliyo katika kurasa za ndanio zatamthiliya hii.Kilio chetuni kilio cha jamii nzima kuhusu gonjwa la UKIMWI. UKIMWI umepoteza maisha ya watoto, vijana, wazazi na ndugu zetu ambao ni muhimu sana kwa ustawi wa familia na jamii kwa ujumla.
Kilio chetu kama jamii ni muhimu ili kuonesha huzuni yetu dhidi ya gonjwa hili la UKIMWI ili jamii isiendelee kuwa na kilio.
Kwa ujumal, kilio chetu ni jina la kitabu ambalo lina sadifu yaliyo ndani kwa namna mbili.
  1. Kilio chetu” ni kielelezo cha huzuni walizonazo wahusika ndani ya kitabu kutokana na ugonjwa wa UKIMWI kuathiri watu wengi.
  2. Kilio chetu” pia inawakilisha mahitaji au matakwa ya kuwepo kwa elimu ya UKIMWI na Jinsia ili kupambana na UKUIMWI.
Hivyo, Kilio chetu imesadifu yaliyomo ndani ya kitabu kwa kuonesha vilio vinavyotokana na UKIMWI na pia vilio vya kuhitaji msaada madhara ya UKIMWI.
KUFAULU N A KUTOFAULU KWA MWANDISHI
  1. Kufaulu
Kimudhui, mwandishi amefaulu kueleza jamii UKIMWI ni kitu gani, njia zinazoambukiza na kujikinga na namna ya kuhudumia wagonjwa wa UKIMWI. Mwandishiamesisitiza umuhimu wa Elimu, uwazi na ukweli kama mbinu muhimu ili kuvunja ukimva.
Kifani, mwandishi ameweza kuumba wahusika wa rika tofauti amabao ni muhimu katika kupambana na UKIMWI
B. Kutofaulu
Mwandishi ameonesha vijana ndio waathirika pekee wa UKIMWI. Mwandishi angeweza kwenda mbali zaidi kuwa watu wazima, na hata baadhi ya watu wanonesha kama watakatifu wanaweza kuwa chanzo cha UKIMWI. Mwandishi angeweza kugusa hata ndoa. Namna watu wanavyopaswa kulinda na kuheshimu ndoa zao ili kuepuka UKIMWI. Mama wajawazito wangehimizwa zaidi kupima virusi ili kuwa namna ya kumsaidia kiumbe aliye tumboni. Si wote wenye UKIMWI hupata kwa njia ya ngono, kuna wengine hupata virusi vya UKIMWI kwa njia nyingine.

NADHARIA NA UHAKIKI WA USHAIRI
Jina la kitabu – MALENGA WAPYA
Waandishi – TAKILUKI
Wachapishaji – OUP

Utangulizi
Malenga wapya ni kitabu kinachozungumzia masuala mbalimbali ya kijamii kama vile ukombozi wa mwanamke, umuhimu wa Kilimo,
umuhimu wa kutatua matatizo katika jamii, umuhimu wa kutenda mema, matumizi mazuri ya pesa pamoja na athari za ukoloni mamboleo.
Maudhui
Dhamiri kuu: Ukombozi
Katika diwani hii msanii amejadili dhamira ya ukombozi wa kiuchumi, kisiasa, kitamaduni na kifikra.
Ukombozi wa Kiuchumi
Katika kujadili ukombozi wa kichumi msanii amesisitiza mambo muhimu yafuatayo:
Kwanza, Umuhimu, wa kuinua uchumi wetu. Katika suala la kuinua uchumi wa nchi yetu wasanii wanasema kuwa kuna umuhimu wa kujenga uchumi imara ili kujenga taifa lenye uwezo wa kujitengemea kiuchumi.
Katika shairi la “Tuzingatie Haya,” (uk .27 – 28) wasanii wanasisitiza umuhimu wa kufufua uchumi wa nchi. Pia ili tufufue uchumi wa nchi ni lazima tupunguze maneno na sote tufanye kazi kwa bidii, wananchi wote tuungane na kuhamasishwa (ubeti 2.) raia na viongozi sote tufanye kazi kwa bidii (ubeti 3) tuondoe tofauti zetu za tuepukane na tamaa ya utajiri. Beti za (2 na 4) zinasema:
2. Uchumi kufufua, si hotuba refu sana.
Moja litosaidia, ni kuhamasishana,
Jingine linalofuatia, sote kushirikiana,
Tuyazingatie haya, wala tusirudi nyuma.
4. Kufanya kazi lazima, tuacheni utegezi,
Na jingine la kukoma, kuwepo kwa uchaguzi,
Kutupiana lawama ni mambo ya kipuuzi,
Tuyazingatie haya, wala tusirudi nyuma.
Hapa inaonekana kuwa ili tuweze kuinua uchumi wa nchi ni lazima tuwahamasishe watu; tujenge umoja na ushirikiano, tuondoe ubaguzi na tufanye kazi kwa bidii.
Shairi hili, pamoja na mambo mengine linawataka viongozi waache kupora mali ya umma na badala yake washiriki barabara katika kujenga uchumi. Iwapo tutajenga uchumi imara tutaondokana na mtatizo yanayoonekana.Haya tunayapata katika shairi la Tunzo (uk.29 – 30).
Jambo la pili ambalo wasanii wanalisisitiza katika ukombozi wa kiuchumi ni umuhimu wa Kilimo.Wasanii wanasema kuwa iwapo tutazingatia Kilimo tutapata chakula cha kutosha na ziada ya kuuza nje ya nchi kwa ajili ya kujipatia pesa za kigeni na kwa ajili ya kuboresha maisha yetu. Iwapo utazingatia Kilimo tutaepukana na tabia au hali ya kutegemea chakula kutoka nje. Suala la kupata chakula cha kutosha litatuepusha na masharti magumu yanayoweza kupewa na watu wanaoweza kutupatia chakula pindi tunapopata tatizo la uhaba wa chakula.
Washairi wanadhihirisha haya kwa kutumia shairi la Adui (uk. 13)
4. Tulime jama tulime, tushinde adui njaa,
Hapa kwetu ituhame, kwingine kutokomea,
Wala sisi tusikome,, chakula kujilimia,
Tutie jembe mpini, tuteremke shambani

5. Chakula kujilimia, ziada kujipatatia,
Tuache kutegemea, vya nje kuagiza,
Siku watojigomea, nani tutamkimbilia
Tutie jembe mpini, tuteremke shambani
Katika shairi la “Mkulima” (uk. 3 – 4) linaonyesha mkulima kama mtu duni likimlinganisha na watu wengine. Huyu ni mtu ambaye analima ili kulisha watu wote nchini na kuinua pato la taifa, lakini hathaminiwi na watu wanaohusika.

5. Wakazi wa mjini, na wafanyakazi pia,
Na viongozi nchini, huduma awapatia.
Sijui kukosa nini, thamani kutomtia,
Mkulima naye mtu, yafaa kuthaminiwa
Hivyo basi, ili tuimarishe Kilimo ni lazima kumthamini mkulima. Na kumpa huduma muhimu anazostahili. Pia chakula kipunguapo nchini wa kutupiwa lawama ni mkulima ambaye hathaminiwi. Wanasema:
7. Upungufu wa chakula, utokeapo nchini,
Hukumbana na suala, shambani wafanya nini,
Kazi yako unalala, watia njaa nchini,
Mkulima naye mtu, yafaa kuthaminiwa.
Licha ya Mkulima kufanya juhudi kubwa katika kuinua uchumi wa nchi hapewi huduma muhimu, badala yake huduma hizo hupelekwa mjini; Kama wanasemavyo waandishi;
8. Starehe kwa jumla, zinaishia mjini,
Maji safi ya muala, njia na umeme ndani,
Aliyezichuma hela, ni Mkulima shambani,
Mkulima naye mtu, yafaa kuthaminiwa.
Hapa inaonyesha kuwa licha ya kwamba mkulima ndiye anayezalisha kila kitu.Wanaofaidi matunda ya Mkulima ni watu wa mjini. Ili tuweze kuinua na kuimarisha Kilimo chetu, ni lazima tumthamini mkulima na apewe misaada na huduma mbalimbali.
Kwa upande mwingine wasanii wanaonesha kuwa ili tuweze kujikomboa kiuchumi ni lazima tuachane na uzembe kazini. Washairi wanadai kuwa kuna baadhi ya watu hasa, wafanyakazi maofisini ni wazembe ,hawatimizi wajibu wao kama ipasavyo.pindi tu waingiapo ofisini wanajifanya wana kazi nyingi kiasi kwamba kiasi kwamba wanashindwa kuwahudumia wananchi kama wasemavyo washairi katika shairi la Puuzo (uk. 8).
  1. Ofisini ukifika, wanajitia pirika,
Haja unayoitaka, mwenyewe tuhangaika,
Wajifanya hawajali
4. Baoni utapokaa, mwishowe tapakataa
Shida iliyokukaa, nayo yazidi chakaa,
Sababu puuzo zao
Wasanii hawa wanakemea tabia hiyo na kuwataka wanajamii wachape kazi kwa bidii ili kuinua uchumi wa nchi. Uchapaji kazi huo lazima uanzie katika

ngazi ya chini kama vile familia, hadi kitaifa. Wafanyakazi, wakulima na wasomi wote sharti wachape kazi kulingana na majukumu yao ili kuteketeza adui

uzembe. Haya tunayapata katika shairi la Charuka (uk. 53 – 55).

Vilevile wasanii wanonesha kuwa ili tujikomboe kiuchumi tupige vita ukoloni mamboleo na unyonyaji. Ukoloni mamboleo ni hali ya nchi moja kuitawala

nchi nyingine kiuchumi. Hii inaathiri uchumi wa nchi maskini. Katika shairi la “22” Nipatieni Dawa,” jinsi ukoloni ulivyoondoka nchini inazungumzwa

lakini ukoloni huo umerudi kwa umbo lingine la ukoloni mamboleo. Kuja kwa ukoloni mamboleo, kuliendeleza taratibu na desturi za kunyonya uchumi wa

nchi masikini.
6. Pale pale penye donda, ndipo apojanibana.
Nikawa sasa nakonda, pumzi nikawa sina,
Nikabaki kama ng’onda, la kufanya sikuona,
Nipatieni dawa, nipate kutononoka.
7. Kila nikifurukuta, donda apate toa,
Najuta kwenye tata, shina kujizidishia
Dawa nimeshatafuta, ili nipate kutoa,
Nipatieni dawa, nipate kutononoka.
Beti hizi zinaweka wazi jinsi ukoloni mamboleo unavyozibana nchi maskini kiuchumi
mpaka zinashindwa hata kupumua. Ili tujikomboe kiuchumi, ni lazima tufate dawa ya kuondoka ukoloni mamboleo hapa nchini. Kwa hiyo ili tujikomboe kiuchumi lazima tupege vita ukoloni mamboleo.
Ukombozi wa kiutamaduni
Katika ukombozi wa kiutamaduni wasanii wanazungumzia juu ya ukombozi wa mwanamke. Ukombozi wa mwanamke ni jambo la msingi na muhimu katika jamii. Mwanamke akikombolewa ni sawa na jamii nzima kukombolewa. Shairi la 10, “Kifungo”, waandishi wanasema;
7. Kwa kuwa ni mwanamke, ndani mnanifutika
Lazima nje nitoke, kupata ninayotaka,
Nimechoshwa na upweke, sitaka kudhalilika,
Kifungo kimenichosha, minyororo nafungwa.
Ili aweze kujitegemea mwenyewe, mwanamke anahitaji kuwa huru, na siyo kufugwa fugwa ndani na kumtegemea mwanamme.
“Hina inapapatuka” Linaonyesha jinsi mwanamke alivyogandamizwa na mwanaume hapo zamani:
  1. Zamani tukikumbuka,watiaji walivia,
Nyumbani katu kutoka, ndani walijichimbia,
Mabwana walitamka, marufuku kutembea,
Unyonge inaondoa, Hina inapatikana.
Hapa wanaonyesha kuwa mwanamke hakuruhusiwa kwenda kutembea. Mwanamke aliwekwa utawani na kazi yake kubwa ilikuwa kupika chakula.
Hakuruhusiwa kabisa kusoma na kuandika.
Hata hivyo mabadiliko ya jamii kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni yanamkomboa mwanamke kidogo kidogo. Kwa wakati huu nao wanafanya kazi mbalimbali ambazo hapo zamani hawakuruhusiwa kuzifanya kwa mfano:
7. Leo wanamakanika, hadhi yao kutetea,
Kila mahali kufika, na wao wameenea,
Kazini wajumuika, shime wanajifanyia.
Unyonge inaondoa, hina inapapatuka.
8. Kila utapopashika, nao wameshafika,
Zege inapopondeka, ni wao hujipondea,
Matofali kupeleka, mafundi kusaidia,
Unyonge inaondoa, hina inapapatuka.
Kujikomboa kwa mwanamke kunatokana na juhudi zake chini ya Umoja wa Wanawake ambao umewaongoza wanawake katika kudai haki zoa na kuondoa dhuluma wanazofanyiwa na wanaume (ubeti 6).
Kwa sasa, wanawake wanajua kusoma na kuandika (ubeti 9) wengine wamejiunga na jeshi (ubeti 11) na wengine ni viongozi (ubeti wa 10).
Tena wananasisitiza kuwa, wanawake washikilie uzi walio nao. Wasipunguze mkazo bali wakazane ili waufikie ukombozi wa kweli, utakaowapa uhuru wa kuamua mambo yao wenyewe bila kuingiliwa na wanaume (ubeti 14).
Ukombozi wa Kisiasa
Katika shairi la “Samaki Mtungoni,” (uk. 19) linaonyesha harakati za watu wa tabaka la chini kuondokana na utumwa wa kutawaliwa na kugandamizwa na mkoloni. Samaki anaashiria watu wa tabaka la chini wanaonyonwa na kugandamizwa; Na mvuvi ni wakoloni au tabaka tawala.
Ukombozi wa Kifikra
Katika shairi la “Usiwe Bendera” (uk. 31) linazungumzia juu ya ukombozi wa kifikra na kimawazo.jamii inatahadhariswa isiwe bendera kufuata kila uelekeo wa upepo bali ijitegemee kimawazo.
Dhamira nyinginezo.
  1. Matabaka
Samaki Mtungozi” linaonyesha matabaka ya aina mbili: tabaka la chini (samaki) na tabaka tawala (mvuvi). Tabaka tawala linanyonya na kulingandamiza tabaka tawaliwa.
Shairi la 14, “Punda” waandishi wanaonyesha jinsi tabaka la chini linavyotumikishwa kwa kulinganishwa na punda.
Nini Wanagu” inaonyesha hali ya maisha ilivyongumu na duni kwa tabaka hili la chini ambalo halina kitu, ukilinganisha na tabaka la juu.
Shairi 2,”mkulima” linaonyesha jinsi mkulima asivyothaminiwa na tabaka la juu (viongozi).Mpaka inafikia hatua ya kumyima hata huduma muhimu anazo ta kiwa kuzipata.
  1. Uongozi mbaya
Katika kujadili dhamira hii waandishi wameonyesha kuwa uongozi uliopo hauwajibiki na hivyo ni mbaya.
Shairi la 5 “Puuzo” linazungumzia jinsi viongozi wasivyotoa huduma zinazotakiwa maofisini mwao, badala yake husumbua watu wanaohitaji huduma hizo:
2. Unapokuwa na shida, wao wanakupuuza
Watajitia kidada, na kuifanya ajiza,
Wajifanya hawajali.
3. Ofisini ukifika, wanakuweka baoni
Wakati uliofika, wao hawathamini,
Wanakwambia subiri.
Shairi la 4, “Bahari’ inazungumzia jinsi viongozi wanavyowadhulumu raia haki zao:
7. Hudai ni haki yao, Mola amewajalia.
Kuwadhulumu wenzao, wao wanafurahia,
Nao kwa unyonge wao, wadogo wateketea,
Bahari ina hatari, wala usiichezee.
Mpaka Lini” inahusu jinsi viongozi wamejitia uziwi ili wasisikilize matatizo ya raia na wasivyotatua matatizo yao. Viongozi huwakumbatia wasema uongo na wasema kweli hunyanyasika.
Katika shairi la 32. “Payuka” wasanii wanaonyesha jinsi viongozi wetu wanavyopayuka ovyo na kuahidi mambo mengi wakiwa jukwaani lakini hawatekelezi yale wanayoongelea. Badala yake,wanabaki kuwaonya na kuwanyanyasa wananchi.
  1. Umuhimu wa kutatua matatizo katika jamii
Matatizo ya jamii ni mengi mno hasa baada ya kupata uhuru wa bendera. Hivyo ni vyema yashughulikiwe ili kuepusha migongano na majungu ambayo yanaweza kujitokeza na kuchukua sehemu kubwa ya muda wa kujenga nchi yetu.
Shiri la 19. “Tunzo,” wasanii wanazungumzia umuhimu wa kutatua matatizo mbalimbali katika jamii yetu ili tuweze kuishi kwa Amani. Matatizo ni kama vile, ongezeko la watu (ubeti 2), kuanguka kwa uchumi (ubeti 3) maradhi mbalimbali (ubeti 3), ubaguzi (ubeti 4) n.k. matatizo hayo yanatatuliwa kwa ushirikaino wa watu wote katika jamii:
6. Kwenu ninalo tamko, kwa yote jamii nzima fuatizo,
Sote tuwe unganiko, kina baba kina mama ni himizo
Tuondoshe sawijiko, ili yapate tuhuma matatizo.
7. Tuyatende kwa pangiko, ili yasije tukwama mzozo,.
Tufanye kimzunguko, vijana watu wazima saidizo,
Tulipata ongezeko, la mazao yenye nema na uwezo.
  1. Mapenzi na ndoa
Katika kuongelea suala la mapenzi wasanii wamejaribu kugusia hata mapenzi ya watu wawili ambao tayari wako katika ndoa. Katika kujadili suala hili la mapenzi msanii anaanza kumsifia mwanamke ampendaye. Wanasema kuwa mwanamke huyo ni mzuri sana kiasi kwamba kila mtu huvutiwa na uzuri wake. Haya yanadhihirishwa na shairi la Ua (uk. 21 – 22) lisemalo,
3. Rangi yake ya sanaa, machoni inavutia
Ukiliona lang’aa, moyoni lakuingia,
Ua sasa limejaa, macho walikodolea.
Wasanii wanadai kuwa ataendelea kumpatia matunzo ili wengine wasimpatie na hatimaye awe mwenzi wake siku itakapofika. Wasanii wanasema,
7. Nami sitoliachia, matunzo talipatia,
Hadi nitapofikia, mkononi kulitia,
Ua sasa limepea, macho walikodolea
Kutokana na mapenzi ya dhati aliyonayo mshairi huyo, anatoa majonzi yake kwa mwenza wake aliyeishi naye kwa muda wa miaka sita kabla ya kifo kumchukua. Anadai kuwa mpendwa wake huyo alikuwa na tabia nzuri na hakuwa na matatizo yoyote. Haya yote yanadhihirishwa na shairi la Nipate Wapi Mwingine (UK. 32 – 33),
  1. Njiwa ali maridadi, kwa tabia hana shaka,
Na hakuwa mkaidi, umwitapo kakufika,
Mfanowe kama radi, chini inapoanguka,
Njiwa ameshanitoka, nipate wapi mwingine?
Hata hivyo, washairi hawa anakemea mapenzi yasiyo ya kweli, yaani wanalaani mapenzi yasio ya dhati. Wanasema kuwa kuna baadhi ya wanaume hawana mapenzi ya dhati kwa wake zao. Watu hawa huwaacha wake zao na kuvinjari na vimada. Shairi la kwa nini? (Uk. 1 – 2) linadhihirisha haya

4. Mke wake, atamwacha,singizini,
Atoroke, parakacha, migombani,
Kumbe kake, anakochani, mwa jirani,
Kwa nini?
Wasanii wanaendelea kulaumu mapenzi ya ulaghai katika mashairi ya kuunge (uk. 25) utanikumbuka (uk. 44) na Kitendawili (uk. 14). katika shairi la kuunge wasanii wanasema kuwa katu hawakubali kushiriki na mtu asiye na msimamo katika mapenzi. Anasema:
2. Silipandi asilani, gogo lilokauka,
Naraduwa kuwa chini, japo nitahangaika,
Mnaosema semeni, kisha mutapumzika.
Wasanii wanasema kuwa hawataki mtu kama huyu ili kuepuka maafa ya kimapenzi ambayo yamewahi kuwapata wengine.
Vilevile, katika shairi la Kitendawili, wasanii wanaendelea kulaumu tabia ya baadhi ya watu ambao hawatuliii katika mapenzi yaani wanafanana na jongoo ambaye hawezi kutulia kwa mfugaji wake.
Pia, katika shairi la “Utanikumbuka” mshairi anamwambia mpenzi wake ambaye amemsaliti kuwa atamkumbuka siku za badayae kutokana na ukweli kuwa msanii alishamtendea mambo mengi sana ambaye aliyemlaghai hataweza kumtendea. Anasema.
3.Umeona bora kitu,ukasahau ya nyuma,
Umetupa mbali utu, na zote zangu h
uruma,
Kwako kutokaa katu, ipo siku utakwama,
Utaumiza uwatu, iwe na yako hatima.
Kupiga vita unyonyaji
Wasanii wa diwani hii wanaosha kuwa katika jamii yetu kuna unyonyaji wa hali ya juu kama ilivyokuwa enzi za ukoloni. Katika shairi la Bahari (uk 6 – 7) linaonesha waziwazi jinsi viongozi wanavyowanyonya watawaliwa. Shairi hili linasema.
6. Suala wajiuliza, katika jamii zao,
Wanaona miiujiza, wanayotenda wenzao,
Wakubwa wanajiweza, kula wadogo zao,
Bahari ina hatari wala usichezee.
Shairi hili linaendelea kudai kuwa kitendo cha viongozi kuwanyonya wazalishaji mali mumehalalishwa na viongozi wenyewe. Viongozi wanaona kuwa kunyonya wananchi wakawaida ni haki ya msingi waliyopewa na mwenyezi Mungu. Kitendo ambacho washairi wanakataa. Washairi wanaonesha unyonyaji wa aina hii katika shairi la “Samaki Mtungoni” (Uk. 19 – 20) .katika shairi hili tunaona samaki (watawaliwa) wakinyanyaswa, kuuliwa na kunyonywa na mvuvi (mkoloni au mtawala).Hali hii imesababisha kutoweka kwa utu wa samaki (watawaliwa) kama asemavyo mshairi.
5. Haki yao mepotea, na heshima kuondoka,
Mebaki waninginia, mtungoni mepangika,
Bwana amechachama, nyumba kwenda kupika,
Leo wako mtongoni, huzuni inawakumba.
Washairi wanadai kuwa, pamoja na kuondoa ukoloni nchini, bado hali za wa nanchi wa kawaida ni mbaya sana. Haya yote tunayopata katika shairi la “Hali Halsi” uk. 5) ambalo linaonesha hali tete kwa mwananchi wa kawaid
4. Nuru tuliieneza, giza kulitokomeza,
Wote wasiojiweza, hali kuzifananiza,
Mshumaa unawaka, giza mbona limezidi?
Kwa vile hali za wananchi zinazidi kuwa mbaya tangu enzi za mkoloni hadi leo, washairi wanawataka wanajamii wafanye mapinduzi ya kweli dhidi ya unyonyaji na ukoloni wa aina yoyote. Haya yote yanapatikana katika mshairi ya Sokomoko baharini (uk. 63 – 64) Haki (uk 47 – 48) na Payuka (uk 50 – 52). Mashairi haya yote yanatoa mwamko wa kisiasa, mwamko wa kuleta mabadiliko katika jamii ili haki ipatikana”.Katika shairi la Sokomoko Baharini, mshairi anakusanya vijana na wanyonywaji ili waungane kwa pamoja na kwa lengo la kuleta mabadiliko. Anasema,
10. Hapa mbele sirudi tena, nia mimi nimechukiwa,
Nenda kusanya vijana, hali wanaoijuwa,
Matumbo yalokunjana, wa tayari kuambiwa,
Mashua kuiokoa, mbio watakimbia.
Shairi la Haki linaendelea kuamsha mioyo ya wanyonge ili wapambane dhidi ya unyonyaji na ukoloni, Shairi hili linawataka wanajamii watafute haki yao ambayo imetekwa na watawala wao. Shairi linasema
8. Haki husimama, kwa Viumbe sisi, tuvyojaaliwa,
Na huna ulimi, kuweza tukasi, tukageukiwa,
Zama za uchumi, zishashika kasi, nguvu zishapewa,
Haki wauliwa
Mashairi hayo yanafanana na utenzi wa Payuka unaowataka wanajamii wamke na kupigania haki zao ambazo zimevizwa na baadhi ya watu kama vile watawala wao au wakoloni. Utenzi huu unasema,
16. Amkeni amkeni,
Msilale asilani,
Vibaya mnaumia
6.Maadili mema na maonyo katika maisha.
Katika diwani hii, wasanii wamejaribu kuwaadili na kuwaonya wanajamii ili waweze kuishi maisha bora. Katika kuzungumzia suala hili, wasanii amegusia masuala yafuatayo:
Moja, matumizi mazuri ya fedha. Wasanii wanaitaka jamii kutumia vizuri pesa inazozipata. Wasanii wanasema kuwa iwapo jamii itatumia pesa zake vibaya itakuja kujuta siku za baadaye. Wanajamii wanatakiwa kutunza pesa vizuri ili kujenga maisha yao ya baadaye. Haya tunayapata katika utenzi wa Israfu (u. 17 – 18).
6. Huu ni wakati wako,
Kujenga kesho yako,
Kuepuka chokochoko,
Za hao adui zako,
Mwenzangu nakuisia, Israfu haifai.
Hivyo, tutumie vizuri fedha zetu ili kuepukana na majonzi au majuto tunayoweza kuyapata siku za baadaye.
Mbili, umuhimu wa kusema ukweli, Wasanii wanawataka wanajamii kusema ukweli daima. Katika shairi la Ulimi (uk. 41) wasanii wanaziasa ndimi zao tusiropoke bali ziseme ukweli tupu. Hali hii itasaidia kulinda heshima yao katika jamii. Shairi hili linasema.
3. Usiropokeropoke, kwa wenzio kwanza sema,
Usipachikepachike, maneno yasiyo mema,
Useme wanufaike, kwa kauli yako njema.
Ewe ulimi sikia!
Wasanii wanaendelea kudai kuwa kwa vile ulimwengu umejaa shida, lakini shida hizo zisiwe chanzo cha kusema uongo.Hayo tunayapata katika shairi la Ulimwengu (uk. 42 – 43) ubeti wa 3.
Shida dhiki ni halali, haramu ikijibari,
Ni bora kutoa kweli, uongo uso wa nari,
Ni vyema kutakabali dhila na zake hatari,
Ulimwengu!
Ukweli husaidia kujenga jamii iliyo bora, husaidia kuondoa wale wote wenye nia ya kubaguana, hasa katika masuala ya dini, rangi na hata kabila. Haya yote tunayapata katika shairi la Pasua Uwape Ukweli. (uk 46).
Nalo shairi la “Mwabwaja Mwasema Nini”? (uk. 61 – 62) linadhihirisha dhana ya kusema ukweli kwa kuwataka watu waseme ukweli kwa vitendo. Washairi wanawataka waandishi waseme ukweli kuhusu hali halisi ya maisha ya watu wa kawaida. Vilevile, anawataka waandishi watekeleze kwa vitendo wanayoyasema. Kusema ukweli na kutenda mambo yasemwayo itasaidia sana katika kujenga jamii iliyo bora.
Tatu, umuhimu wa kutenda mema. Wasanii, wanawausia wana jamii kutenda mema kwani mtu yeyote atendewaye mema anastahili kulipa kwa wema aliotendewa, hata kwa kusema ahsante. Na yeyote atendaye mema atalipwa kwa njia yoyote ile, ikiwemo ya kiroho. Katika shairi la “Hisani Hulipwa” (uk. 45) tunaambiwa kuwa,
3. Akufichiae,siri, zinonuka,
Na akurambae, akakusafisha,
Akutafutae, unapopotea,
Hisani hulipwa.
Nne ,ni kuachana na anasa za dunia.Wasanii wanawaasa wanajamii kuachana na tamaa za kimaisha. Shairi la Siharakie Maisha (uk 11 – 12) linawaasa wanafunzi kuachana na papara za kimaisha na badala yake wasome kwani maisha ni kama kupanda mnazi ambapo mpandaji sharti aanzie shinani kama atakiwavyo mwanafunzi kutong’ang’ania mambo ya anasa za dunia kama vile umalaya, ulevi, uchoyo, wizi n.k. bali ajijengee ya kesho, yaani asome kwa bidii ili apate elimu bora ambayo ndio msingi wake wa maisha ya baadaye. Shairi hili linasema,
2. Ubado ni mwanafunzi,
Usingiwe na simanzi,
Ruka vikwazo ja panzi,
Ipambe yako enzi,
Maisha safari ndefu, kutembea usichoke.
3. Somo babo endelea,
Sicheze pata potea,
Muda wako ukimea,
Maisha kufurahia,
Usiache kutegua, kwa kutegemea tega
Wasanii wanaendelea kudai kuwa raha za dunia hazina thamani kwani waliowahi kupata raha sasa wanajuta. Wanaonesha kuwa watu hao pindi wapatapo pesa huwasahau wengine kwa kuwaona kama hawafai huyafakamia maisha kabla dunia haijawafundisha. Haya yote tunayapata katika shairi la Raha (uk – 24) ambapo mponda raha anajuta,
4. Leo raha naiwacha, atakaye aje kwetu,
Nami nataka kututa, nitulie kama watu,
Nimechoka kuzorota, nakubakia sukutu,
Chukueni mtumie.
7.Umuhimu wa kutumia pesa vizuri.
Matumizi mabaya ya fedha ni kujitia kwenye umasikini, na mali bila daftari hupotea bila kujua. Katia diwani hii, waandishi wanaonyesha au wanasisitiza juu ya matumizi mazuri ya pesa.
Katika shairi la 11, “Israfu” wasanii wanaionya jamii juu ya matumizi mabaya ya fedha zinazopatikana:
1. Mali ulijichumia,
Ni yako nakubalia,
Lakini kuangalia,
Vipi unaitumia,
Mwenzangu nakuusia Israfu haifai.
Wasanii wanaonyesha kuwa matumizi mabaya ya fedha husababisha umasikini kwa muhusika na umaskini husababisha akimbiwe na watu wote hata marafiki zake.
8. Athari ya sukari mwilini
Sukari ni kitu cha muhimu sana katika mwili wa binadamu. Lakini sukari hiyohiyo ikizidi inaleta madhara mbalimbali mwilini.
Katika shairi la 34 “Sukari” Wasanii wanaonyesha madhara mbalimbali yatokanayo na sukari kuzidi katika mwili wa mwanadamu. Athari hizo ni kama vile meno kung’oka (ubeti 2)
Pia sukari huleta safura mwilini na ugonjwa wa kisukari.
Ujumbe (Maadili mabalimbali)
1. Kuinua uchumi wa nchi ni jambo la muhimu sana, ili tuweze kuondokana na utegemezi wa kutegemea misaada toka nje.
2. Kilimo ni uti wa mgongo wa uchumi wetu, hivyo ni lazima tukiimarishe na Mkulima lazima athaminiwe.
3.Ukombozi wa mwanamke ni muhimu sana, kwani mwanamke akikombolewa atazijua na kudai haki zake kwa ujasiri,na atakuwa msaada mkubwa zaidi kwa jamii.
4. Ni muhimu kutatua matatizo mbalimbali yanayoikabili jamii yetu ili tuweze kuishi kwa Amani na utulivu.
5. Ni vizuri kuwa na maadili yaletayo kutendeana mema katika jamii, kwani kufanya hivyo tutajenga jamii yenye haki na usawa.
6. Ni vizuri kuwa na matumizi mazuri ya pesa zetu ili kuukwepa umasikini.

Falsafa (Mwelekeo)ya Waandishi
Waandishi wanaamini kuwa tukisisitiza Kilimo na kumthamini mkulima tutainua uchumi wetu kwa kiasi kikubwa. Pia wanaitaka jamii ifuate misingi ya haki na usawa katika maisha. Wanatetea haki na usawa kwa watu wote.

Msimamo wa Wandishi
Waandishi wana msimamo wa kimapinduzi kwani wamejadili masuala mbalimbali ambayo ni nyeti kwa jamii yetu na kukemea uonevu kwa ujumla.
Fani
Muundo
Miundo changamano umetumika. Kuna muundo wa tathlitha (mistari mitatu)- shairi la 5 “Puuzo” 13 “Ua,” na 32 “Payuka”: tarbia (mistari minne) – shairi la 4 “Bahari”/ 2 “Mkulima” 20 “Usiwe Bendera” 27 “Utanikumbuka” na sabilia au takhmisa (mistri mitano na kuendela) shairi la 7 “Siharakishe Maisha”/“11 Israfu” na 14 “Punda”.
  • Mtindo
Waandishi wametumia mtindo unaofuata kanuni za ushairi wa kimapokea na urari wa vina na mizani kwa mshairi mengi, mfano shairi la 2,3,4,6,8,9,10,12, n.k. Pia wametumia mtindo unaofuata ushairi wa kisiasa kwa mfano katika shairi la 19.
Matumizi ya Lugha.
Lugha waliyoitumia waandishi ni ya kishairi yenye methali, tamadhali za semi, mbinu nyingine za kisanaa na taswira mbalimbali.
Methali
  • Subira yavuta heri (shairi la 7 ubeti 8)
  • Aisifuye mvua kaloa mwilini mwake (shairi la 23 ubeti 12)
  • Fahari wapiganapo nyasi ndizo huonewa (shairi la 37 ubeti 7)
  • Misemo:
  • Siharakie maisha (shairi la 7).
  • Kusumbukia kichaa (shairi la 23).
  • Sokomoko baharini (shairi la 37).

  • Tamathali za semi
  • Tushibiha
Ubaguzi umezama kama nguzo (shairi la 19 ubeti 4).
Maisha ni kama njia (shairi la 24).
  • Tashihisi.
-Katika shairi la “Samaki Mtungoni” Samaki wamepewa uwezo wa kibinadamu.
-Katika shairi la “Nipate Wapi Mwingine”. Hapa njiwa amepewa uhai kama mpenzi aliyefariki.
  • Mbinu Nyingine za Kisanaa.
  • Tashtiti – katika shairi la “Mwabaja Mwasema Nini?” mfano– Nasikia mnatunga, mwatungani washairi?
  • Tanakali sauti – mfano katika shairi la “Kwa Nini”! – neno parakacha, shairi la “Mkulima” neno kokoriko n.k.
  • Takriri – kuna matumizi kurudiarudia maneno katika mashairi ya “Kifungo” – “Adui” “Majonzi” n.k
Ujenzi wa Taswira
Njiwa – Mpenzi -katika shairi la “Nipate Wapi Mwingine?’
Samaki – Watu wa tabaka la chini
Mvuvi – Watu wa tabaka tawala – shairi la “Samaki Mtungoni
Punda – Tabaka la chini linalonyonywa na kuagandamizwa
Ua – Mwanamke au msichana.
  • Jina la Kitabu
Jina la diwani hii , Malenga Wapya linaendana na makusudio ya watunzi. Neno malenga lina maana ya mshairi na neno wapya lina maana ya watu au vitu ambao au ambavyo ni wa / vya kisasa. Hivyo Malenga Wapya lina maana ya washairi wapya. Hali hii inatufanya tuamini kuwa jina Malenga Wapya linaendana na hali halisi ya mambo yaliyo ndani ya diwani hii kwa kuzingatia nyanja kuu, mbili:
Kwanza katika utangulizi tunaambiwa kuwa Malenga Wapya ni mkusanyiko wa mashairi 37 yaliyotungwa na wanafunzi mbalimbai katika kipingi cha uwanafunzi wao (uk. 5) kwa maneno mengine Malenga Wapya lina maana ya washairi wapya au washairi vijana (wachanga) walioamua kuingia katika uwanja wa ushairi.
Pili, malenga wapya lina maana ya washairi wapya wanaotumia mitindo mipya ambayo imo ndani ya diwani hii. Kusema ukweli diwani hii ina upya fulani, hasa kwa upande wa mtindo. Upya huu ni nadra kuupata katika diwani nyingine, ingawa mtindo uliotumika wa kimapokeo peke yake. Hata hivyo mtindo huu umeibua mshairi yenye mitindo tofautitofauti. Jambo hili linaifanya diwani hii ionekane mpya au ionekane tofauti na diwani tulizowahi kusoma. Upya huu kimtindo, unaweza kuelezwa kama ifuatavyo:
Diwani hii ina baadhi ya mashairi yenye vina viwili vya kati tofauti na diwani zilizo nyingi, ambazo tumewahi kusoma. Kwa mfano, katika shairi la “Tunzo” (uk. 20) tunaona hali hii,
8. Tulete mabadiliko, huku nia iwe njema, tangu mwenzo,
Matumaini yaweko, tukijachagua mema, kimawazo,
Tena aliadi, iweko, kwa nchi yetu nzima, endelezo.
Tukichunguza shairi hili tutaona kuwa kuna vina vya kati vya aina mbili, ambavyo ni “ko” na “ma” kama vinavyoonekana ndani ya shairi. Shairi jingine lenye vina vinavyofanana na hilo ni “Haki” (uk 47 – 48).
Vilevile, kuna upya mwingine katika utumiaji wa mizani. Baadhi ya mashairi kama vile “Usiwe Bendera (uk 31) na Hisani Hulipwa” (uk. 45) yana mizani 12 badala ya 16 au 8 kama ilivyozoeleka katika mashairi ya kawaida na tenzi zenye kufuata kanuni za kimapokeao. Shairi la Usiwe Bendera linathibisha haya,
1.Kaa ufikiri, ni tokueleza,
Haya udhukiri, ukiyachunguza,
Hujawa mazuri, hwenda yakatunza.
Ubeti huu una mizani 12, kwa maana kuwa kila nusu mstari una mizani 6 Mwisho, washairi hawa wametumia mtindo wa tenzi ambao pia una upya fulani. Upya huo unaonekana katika mstari wa mwisho ambao una mizani nyingi tofauti na mistari mingine ya tenzi ambayo kwa kawaida huwa na mizani 8. Lakini mstari wa mwisho una mizani 16. Hali hii inajionesha katika tenzi za Siharakishe Maisha. (Uk 11 – 2) Israfu (uk. 17 – 8). Mfano mmojawapo ni ubeti wa 2 wa utenzi wa Sibarikie Maisha.
Ubado ni mwanafunzi
Usingiwe na simanzi
Ruka vikwazo ja panzi
Uipambe yako enzi,
Maisha safari ndefu, kutembea usichoke.
Tunaweza kusema kuwa ingawa hakuna upya wowote kimaudhui lakini kifani kuna upya mwingi. Upya huu, ikiwa ni pamoja na uchanga wa watunzi au washairi ndio unaotufanya tusema kuwa jina la diwani Malenga Wapya linasadifu yale yaliyomo ndani yake
  • Kufaulu kwa Mwandishi.
Kimaudhui
-Mwandishi amefanikiwa kutuonyesha dhamira mbalimbali ambazo zinaonyesha maisha yetu kabla ya uhuru na baada ya uhuru mpaka sasa.
-Waandishi wameonyesha mvutano kati ya tabaka la chini na tabaka la juu (uongozi mbaya, n.k)
-Wameshauri jamii kuwa na maadili mema.
-Waandishi wameonyesha matatizo mbalimbali yanayoikabili nchi yetu.
Kifani
-Wamefanikiwa kutumia lugha ya kishairi, nyepesi na yenye taswira.
– Kimuundo mashairi yao yanajitosheleza.
Kutofauulu kwa Waandishi
Kimaudhui
-Waandishi katika mashairi ya “Mkulima” na “Adui” wameonyesha ukasuku walionao kwani tangu zamani za kale hadi leo hii watu wamekuwa wakilima lakini bado hali zao ni duni.
-Wamerudiarudia maneno yanayoimbwa majukwaani kuhusu viongozi badala ya
kutuonyesha njia za kisayansi nakiteknolojia za kuondokana na matatizo ya kiuchumi, kifikra na kijamii.,
-Aidha wasanii wamekuwa na mtazamo potofu na dhaifu katika kutoa baadhi ya maadili mfano: shairi la “Hisani Hulipwa
Kifani
Diwani hii imetumia lugha rahisi kiasi kwamba hamfikirikishi msomaji.




Share this:


subscriber

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Accept Our Privacy Terms.*